sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » KATIKA MAZIKO YA ASKOFU MWALUNYUNGU,WAZIRI MKUU ATAKA WATANZANIA WAWE NA HOFU YA MUNGU




                                   
 

Waziri  Mkuu, Mizengo  Pinda akiwa  katika ibada ya maziko ya Askofu Mstaafu wa Jimbo la Tunduru/ Masasi, Magnus Mwalunyungu yaliyofanyia kwenye
kanisa la Tosamaganga mkoani 



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Rais wa Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania, na Askofu wa Jimbo la Iringa, Mhashamu Ngallekumtwa   (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Aina Masenza  baada ya mazishi ya Askofu Mstaafu wa Jimbo la  Tunduru Masasi,  Mhashamu Magnus Mwalunyungu yaliyofanyika kwenye Kanisa la Tosamaganga mkoani Iringa
. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka Watanzania wasikilize na kufuata mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini ili Tanzania iwe nchi yenye watu waadilifu na wenye hofu ya Mungu.

Ametoa wito huo leo mchana  wakati akizungumza na maelfu ya waumini na wananchi waliohudhuria ibada ya mazishi ya Askofu Mstaafu Magnus Mwalunyungu kwenye kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu la Tosamaganga, Jimbo Katoliki la Iringa.

“Leo ni siku ya pekee ya kuwasikiliza viongozi wa dini wakituasa tujiandae kwa maisha baada ya kifo. Tukio hili la leo litupe nguvu ya kukubali kwamba kifo kipo licha ya kuwa hakizoeleki na kinapotokea
kinaleta simanzi kubwa,” alisema.

“Ninawasihi Watanzania wote tufuate mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini zetu ili Tanzania iwe na kundi la watu wenye hofu ya Mungu, waadilifu na wanyofu kama ambavyo mahubiri ya leo
yamesisisitiza,” alisema.





Waziri Mkuu ambaye yuko kwenye ziara ya siku tano ya kikazi mkoani Iringa, aliamua kusitisha ziara yake siku ya leo ili aweze kushiriki msiba huo. Pia alitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete ambaye yuko Kenya kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya
ya Afrika Mashariki.

Akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo, Askofu Damian Dallu wa Jimbo Kuu Katoliki la Songea alisema wanadamu wanahangaika na kuogopa kifo kwa sababu hawajui baada ya kifo maisha yao yatakuwaje.

“Askofu Mwalunyungu ameishi kwa miaka 85 na kati ya hiyo, miaka 55 alikuwa akitumikia kama padre na kwa miaka 22 alimtumikia Mungu akiwa Askofu. Na hata baada ya kustaafu aliomba awe Paroko pale Kidamalai ambako alitumikia kwa miaka minne. Maisha yake yanaendana na neno kutoka kitabu cha hekima kwamba kifo cha mwadilifu ni kupumzika kwa starehe,” alisema.

Ibada hiyo ya mazishi ilihudhuriwa na Maaskofu wa kanisa katoliki zaidi ya 20.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, FEBRUARI 20, 2015.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply