MWANDISHI WA HABARI WILLIAMU BUNDALA AKIHUTUBIA MAELFU YA WAFASI WA CHADEMA KATIKA KATA YA USHETU WILAYANI KAHAMA AMBAPO TUME YA UCHANGUZI IMETANGAZA USHETU NI JIMBO LA UCHANGUZI MWAKA HUU AMBAPO TUMIE IMETANGAZA MAJIMBO 26 MAPYA.
BAADHI YA WANACHNGAZA WA CHADEMA WAKIMBA JUU MGOMBEA WAO WA CHADEMA WILLIAMU BUNDALA BAADA YA KUTANGAZA AZIMA YAKE.
BAADHI YA WANANCHI WA KATA YA USHETU WAKISIKILIZA HOTUBA YA MUWEKA AZIMA Na
Kahama
MWANDISHI WA HABARI HAJITOSA
UBUNGE KAHAMA
MWANDISHI wa habari na mtangazaji
wa Radio Free Africa William Bundala maarufu kwa jina la “kijukuu cha bibi k”
ameamua kuingia
kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo la jipya la Ushetu katika
halmashauri ya wilaya ya Ushetu mkoani Shinyaga,kupitia tiketi ya Chama cha
Demokrasia na maendeleo CHADEMA.
Bundala ametangaza kuingia kwenye mchakato wa
kugombea kuteuliwa na Chama ili aweze kupeperusha bendara katika uchaguzi mkuu
ujao katika mkutano wake wa kutangaza nia uliofanyika katika Kijiji cha Bogomba
“B” kata ya Ubagwe wilayani Kahama.
Mtia nia huyo alisema endapo Chama chake
kitampitisha na hatimaye kushinda Ubunge katika Jimbo hilo atahakikisha
anasukuma kasi ya maendeleo katika jimbo hilo jipya lenye Rasimali nyingi
kupitia nafasi yake na wajibu kama anavyotakiwa Mbunge Kufanya.
Alisema kuwa dhamira yake imemsuta kwenda
kuwatumikia wananchi wa wilaya
hiyo ambayo yeye ni mzawa na kuwa atahakikisha anapigania
maendeleo ya wananchi kwa kasi huku akiondoa uonevu kwa waandishi wa habari na watumishi wengine serikalini na katika halmashauri za
wilaya.
maendeleo ya wananchi kwa kasi huku akiondoa uonevu kwa waandishi wa habari na watumishi wengine serikalini na katika halmashauri za
wilaya.
Sambamba na hayo amesema kuwa sababu nyingine
iliyomsukuma ni kuona wagombea wengine wanaolitaka jimbo hilo hawako kwa ajili
ya ukombozi wa jimbo hilo bali wako kwa ajili ya maslahi binafsi kutokana na asilimia kubwa ya wagombea hao si
wakazi wa eneo hilo na kwamba hawafahamu matatizo ya wana ushetu kama
anavyoyafahamu yeye.
Aliongeza kuwa akifaniiwa kuukwaa Ubunge pia
atasimamia kuhakikisha Jimbo hilo jipya linapata Chuo cha ufundi kwa ajili ya
vijana wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne kupata elimu jambo
lilatalopunguza wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana.
Bundala alisema kipaumbele kingine
atakachoshughulikia ni pamoja na kusimamia na kutoa elimu ya Sheria kupitia
wanasheria ambao watazunguka katika kata kutoa elimu hiyo hususan katika
maswala ya umiliki wa Ardhi,Mirathi,haki za wakulima na wafugaji pamoja na haki
za raia na mali zao kwa ujumla.
Akizungumzia kuhusu suala la michezo katika
jimbo hili Bundala amesema kuwa kupitia Kijukuu Cup atahakikisha anashirikiana
na halmashauri na wadau wa michezo kuhakikisha halmashauri ya ushetu inapata
timu ya kucheza ligi kuu Tanzania Bara.
Awali Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CHADEMA
(BAVICHA) Halmashauri ya Ushetu Emmanuel Magema aliwataka vijana wote kuungana
ili kumuunga mkono kijana mwenzao aliyejitokeza na kuonesha nia ya kutaka
kuongoza akiwa Mbunge wa jimbo hilo.
Wilaya ya Kahama kwa sasa ina halmashauri za wilaya tatu za
Msalala,halmashauri ya mji wa Kahama na halmashauri mpya ya Ushetu na kufanya majimbo ya uchaguzi kuwa matatu.
Katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika jimbo jipya la Ushetu kuna
watu zaidi ya watano wanaotajwa kulimendea jimbo huku wagombea wa CHADEMA
wakionekana kuungwa mkono na makundi mengi hususan vijana
MWISHO
No comments: