sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » USHETU WAKABIDHI MAJENGO YA MAKAO MAKUU KWA MJI HUKU YAKIWA YAMECHAKAA


LICHA ya halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga kukiri kukabidhiwa majengo yaliyokuwa yakitumiwa na hamlamashauri ya Ushetu kama ofisi wakati wakiendelea na ujenzi wa makao makuu huko Nyamilangano lakini majengo hayo yamekabidhiwa rasmi yakiwa yamechakaa huku madirisha ya vioo yakiwa yamevunjwa na watumishi wake hali ambayo nyaraka za ofisi zimezagaa na kuoneka holela.

Hali hiyo ilielezwa na mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Kahama, Abel Shija wakati akizungumza na wandishi wa habari muda mfupi baada ya kamati ya fedha na uchumi kufanya ziara ya kukagua miundo mbinu ya majengo waliyokabidhiwa na kujionea uharibifu uliofanywa na watumishi wa halmashauri hiyo baada ya kugundua wanaondoka huku wakitakiwa kuziacha nyaraka zao.

Shija amewambia wandishi wa habari kuwa kulingana na majengo hayo yaliyokabidhiwa na halmashauri ya Ushetu kwa mji ukarabati wake wake  unahitaji kiasi kikubwa cha fedha hali ambayo  halmashauri itaingia hasara kubwa katika ukarabati wa miundo mbinu wa majengo hayo.  

“Kwa usahihi wa jambo hili kwanza tuishukuru sana serikali kupitia Tamisemi ka sababu imeliona jambo hili lakini pia imewezesha tufante usafi na ukarabati mapema wa majengo haya yaliyokuwa yametelekezwa   pamoja na kurejesha majengo haya yaliyokuwa hapo awali yakitumika kama majengo ya halmashauri ya wilaya ya Kahama na baadaye baada ya kupatikana kwa halmashauri tatu za Ushetu, Msalala na Mji yenyewe, licha ya kukabidhiwa majengo haya wameyaharibu sana kwa kuyachakaza,” amesema Shija mwenyekiti wa halmashauri ya mji.

Pia mwenyekiti huyo amesema kuwa baada ya watumishi wa halmashauri kupata taarifa ya kuondoka katika majengo hayo na kurudi katika makao makuu ya halmashauri yao yaliyoko  katika Kata ya Nyamilangano  badala ya kukabidhi majengo yakiwa na hali nzuri badala yake waliamua kupasua vioo vya madirisha huku nyaraka mbalimbali za ofisi zikionekana jambo ambalo ni hatari.

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kahama Anderson Msumba alisema kuanzia 2014 majengo hayo yalikuwa yamekabidhiwa kwa halmashauri ya mji lakini Ushetu waliomba wakae kwa muda wakati ujenzi wa makao makuu huko Kata ya Nyamilangano unaendelea.

Hata hivyo kwa taarifa za kuaminika kutoka chanzo chetu cha habari wilayani hapa kimesema kuwa kufuatia halmashauri makabidhiano hayo ya makao makuu ya ofisi mjini Kahama baadhi ya Madiwani wa halmashauri ya Ushetu wamepanga kumgawana mkurugenzi mtendaji Michael Matomola na kutishia kumfungia ndani kutokana na amekabidhi majengo hayo bila kushirikisha baraza la Madiwani hao.









Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji Anderson Msumba akimwelekeza mwenyekiti wa halmashauri hiyo , Abel Shija majengo  waliyokabidhiwa na halmashauri ya Ushetu. 

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mji akitoa maelekezo kwa mwenyekiti wa halmashauri ya mji abel Shija.

Ukumbi wa halmashauri ya mji kwaaji ya mikutano na vikao vya halmashauri ya mji ambapo tarehe 12 mwezi huu utatumika .

Muonekano wa majengo ya ofisi yaliyoachwa na halmashauri ya Ushetu na kukabidhiwa halmashauri ya Mji.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply