sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » SERIKALI KAHAMA YADHAMIRIA KUFUFUA ZAO LA PAMBA



Na Mohab Dominick
Kahama
Oct 28, 2013.



KATIKA kuhakikisha zao la Pamba katika Wilaya ya Kahama kwa mwaka ujao  linamnufaisha Mkulima, Serikali Wilayani hapa Mkoani Shinyanga  imepiga marufuku wakulima kutumia mbegu za manyoya na badala yake watumie mbegu kutoka katika kampuni ya Quton.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya alitoa ngalizo hilo katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya maendleo ya Wilaya ya Kahama kilichofanyika juzi Mjini hapa na kuongeza kuwa Mkulima lazime alime kilimo chenye tija kwake kwa wakati huu.

Mpesya alisema kuwa mbegu hizo kutoka Quton ambazo zinaitwa Delinted Seeds ndio kwa sasa zenye tika kubwa kwa Mkulima tofauti na zile za Manyoya ambazo walikuwa wakitumia hapo zamani.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya aliendelea kusema kusema mbegu hizo zinauwezo wa kutoa kilo 1500, kwa heka moja na kuongeza kuwa kwa hali hiyo wakulima wanaweza kupata kiasi cha pamba nyingi kwa kufuata wataalamu wa Kilimo watakaokuwa wakiwaelimisha.

Aliwataka Watendaji wa kata kuhakikisha kuwa Mkulima yeyote katika eneo lake hatmumii Mbegu ya manyoya badala yake watumie mbegu hiyo mpya ambayo ileta mavuno mengi na kuongeza kipato cha Mkulima na kutoa tahadhari kwa yeyote atakayetumia mbegu za zamani apewe taarifa mara moja.

Mpesya alisema pia mbali na mbegu hizo pia wanatarajia kwa mwaka huu Wakulima wa zao la Pamba lazima walime Kilimo cha Mkataba na kuongeza kuwa mpaka kufikia hivi sasa tayari wamwekishapata msaada wa mbegu kwa ajili ya kuzigawa kwa wakulima.

Alisema kuwa kwa Serikali yake Imejipanga katika kuhakikisha kuwa Mkulima wa zao la Pamba anapata faida kubwa kutokna na pamba yake anayolima na kuweza kumudu ukali wa maisha ikiwa ni pamoja na kumudu kuendesha familia yake.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa kwa yale Makampuni ya makapuni ambayo yatakuja ofisini kwake kwa ajili ya kuomba tenda ya kusambaza Pembejeo kwa mwaka huu hayatayavumia kwani hayatapata kabisa.


mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply