sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » VIONGOZI NA MADIWANI WA MJI WADAIWA KUJILIMBIKIZIA VIBANDA.

 Moja ya matangazo ya halmashauri ya mji wa kahama kama livyokutwa na blog hii
 chumba hichi ni mjasilimali ambacho amewekea pingamizi ujenzi wake.
 hivi ndivyo vibanda ambavyo vinalalamikiwa na wafanya biashara wadogo wa hili soko la samanga .
 hivi ndiyo vibandani vya mbele vya soko la samanga ambavyo vimemilikiwa na viongozi  wa halmashauri ya mji na madiwani .
 majengo ya soko la samanga kwa mbele .ambayo kuna baadhi ya viongozi  na madiwa wa halmashauri kujimilikisha kwa mbele .
 tangazo kama hili ndiyo yalivyotukamika kwa wateja walichelewa kufanya matengenezo .
 huku ni nyuma kwenye hili soko la samaga ambalo bado ujenzi wake hukiwa bado kama hunavyonekaka hapo .
 jengo la soko la zamani ambalo limechukuwa zaidi ya miaka mitatu ambapo kumesababisha mvutano mkubwa kati ya wafanyabiasha na madiwani na viongozi wa halmashauri ya mji .
 haya majengo ya soko la samanga ambayo ujenzi wake hunasuasua mpaka sasa kuhusu ujenzi huu na kusababisha msunguano mkubwa .






Na Mohab Dominick
      Sept 11,2014
            Kahama  
WANANCHI Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wamewalalamikia  viongozi wa Halmashauri ya mji wa Kahama pamoja na baadhi ya Madiwani wake kujilimbikizia vibandavya soko la Namanga hali inayowafanya kubaki kuwa wapangaji.

Akiongea juzi na wandishi wa Habari ofisini kwake,katibu mwenezi wa chama cha Tanzania Democratic part Aliance(TADEA) wilayani Kahama,Vicent Manyambo aliwaeleza wandishi wa Habari kuwa wananchi walifika ofisini kwake kulalamika kwa kuwatuhumu viongozi hao pamoja na madiwani wake.

Aidha manyambo alisema kuwa yeye pia ni shuhuda wa hali hiyo na kumtaja mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Felix kimaryo kuwa anamiliki vibanda 6 na wengine ni madiwani wa kata ya kahama mjini, Abass omary kumiliki vibanda 6 Bobson Wambula vibanda 6 kwa jina la mke wake.

Pia alisema mwingine ni Diwani wa kata ya Nyihogo,Amos Sipemba  anamiliki vibanda viwili kutokana na kutokuwa mjanja na mwingine ni aliyekuwa afisa biashara wa mji huo,Boniphace Bulali kuwa naye  anavibanda vyake katika soko hilo na kwamba wajilimbikizia vibanda hivyo na kusababisha wananchi kukosa hali inayowalazimu wawe wapangaji wao.

Hata hivyo manyambo alisema kuwa Halmashauri ya mji huo imekuwa ikiwahamisha kwa nguvu wafanyabiashara hao kutoka katika maeneo yao ya biashara kwakile walichodai kuwa hayo si masoko rasmi ili kuwapeleka katika soko hilo la Namanga ili wawe wapangaji wao.

Alisema mkurugenzi pamoja na madiwani hao wamejilimbikizia vibanda hivyo ambapo wafanyabiashara ambao ndio walengwa hawana vinda katika soko hilo licha ya kumiliki vibanda huko walikotolewa na kwamba wameamua kufikisha malalamiko yao kwa chama hicho ili kiwasaidie.

Akijibu tuhuma hizo Afisa Biashara wa mji huo,Sarah Mlagwa alikanusha madai hayo ya katibu wa TADEA kuwa si ya kweli nakusema kuwa Halmashauri kutokana na tangazo lake la ujenzi wa vibanda wananchi wote waliochukua fomu hizo ndiyo wanaotambuliwa  kuwa ni wamiliki wa vibanda.

Mlagwa alisema hata hivyo baadhi ya watu walijaza fomu hizo walishindwa kukamilisha majengo yao kwa muda uliopangwa na Halmashauri yake ambapo wengi wao waliamua kuviuza kwa watu wenyeuwezo wa kukamilisha kwa muda ulopangwa nakuongeza kuwa hali hiyo ya wananchi kuuza vibanda vyao ilimchanganya katika kuandaa mikataba yao.

Kwa upande wao Madiwani wanotuhumiwa wakiongea na gazeti hili kwa nyakati tofauti wamekanusha madai hayo ambapo wamesema kwamba wao hawana vibanda katika Soko hilo licha ya kuwa baadhi yao wanaishi jirani na soko hilo nakudai kuwa hizo ni chuki binafsi za vyama na kuwachafua kisiasa hasa kwa kuona siku za uchaguzi zimezidi kusogea.

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply