sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » JAMAA AUWA KWA KUKATWA NA JEMBE KICHWANI HUKU AKISHANGILIA USHINDI WA CHADEMA

Kamanda wa polisi wa mkoa wa shinyanga (RPC) justus kamugisha akitolea maelenzo ya vurungu zilizotokea mjini kahama ya moja ya mufasi wa chadema kuwauwa na watu wasiofamika .

Mwanamme mmoja aliyefahamika kwa jina la Simeo Isaka (42),mkazi wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela tarafa ya Mweli  wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, ameuawa kwa kukatwa na jembe kichwani wakati akishangilia matokeo ya ushindi wa mgombea wake kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa  Shinyanga Justus Kamugisha, alisema tukio hilo limetokea Desemba 15 majira ya saa saba usiku wakati mwanamme akishangilia matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa.
Kamanda Kamugisha alisema, marehemu huyo alikuwa  akishangilia ushindi wa mgombea wa Chama Cha Demokrsia na Maendeleo (Chadema), ngazi ya mwenyekiti wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela wilayani Kahama.
Kamanda Kamugisha alisema wakati Simeo Isaka akishangilia ushindi huo  ghafla alivamiwa na watu watatu wasiojulikana  kisha kumkata jembe kichwani, na kisha kukimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Kahama ambako alipoteza maisha.
Kamanda  Kamugisha alisema jeshi la polisi linafanya uchunguzi kuhusu tukio hilo na juhudi za kuwasaka na kuwakamata watuhumiwa wa tukio hilo zinaendelea ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply