RAIS ATOA SIKU 11 KWA MKURUGENZI WA MAMLAKA YA MAJI ANENA HAYA HAPA
by Mohab Dominic-
0
Rais wa jamhuri ya muunganio wa Tanzania Dr. John Pombe Maguful
amesema kuwa haiwezekani watu wa halmashauri ya
Biharamulo wakaendelea kutekeseka wakati serikali imeshawawekea mazingira bora
ya miundombinu, hivyo viongozi wachache wanatakiwa kuwajibika na wakishindwa ni
bora wakajiondoa wenyewe.
Akihutubia mkutano wake katika ziara ya kikazi wilayani Biharamulo, rais
Magufuli amemtaka mkurugenzi wa maji safi na usafi wa mazingiria Bukoba BUWASA,
ambaye ndiye mkurugenzi anayesimamai upatikanaji wa maji katika halmashauri
zinazosimamiwa na serikali katika miundombinu hiyo, kufikia julai 30 mwaka huu
awe amefanikisha upatikanaji wa maji katika halmashauri ya Biharamulo,
vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.