Na
Kahama
Jan
27, 2014.
SERIKALI
imeombwa pindi inapokamata mifugo ya Wafugaji hususani Ng’ombe katika
operesheni zake isichukue jukumu la kuiuwa mifugo hiyo bali wakamatwe wafugaji
na kufikishwa katika vyombo husika vya sheria kujibu tuhuma.
Hayo
yalisemwa juzi na Katibu wa Chama cha Wafugaji Nchini (CCWT) George Kifuko
wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini kahama juu ya epesheni
zilizofanywa na Serikali za kuwaomndoa wafugaji katika maeneo ya Hifadhi.
Kifuko
alisema kuwa kwa sasa Wafugaji wamekuwa na maeneo madogo kwa ajili ya malisho
ya Mifugo huku sehemu kubwa za malisho zilichukuliwa na hifadhi za wanayama
pori hali ambayo inachangia kwa kiasi fualani kwao kuingia katika maeneo hayo.
Alisema
kuwa ni bora kwa sasa Serikali isiwape wawekezaji maeneo pia iangalie upande wa
pili ili na wao pia wawe na maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo yao ambayo
kwa kiasi kikubwa inazidi kuongezeka hasa katika jamii ya wafugaji.
Alisema
kuwa kutokana na operesheni iliyofanyika hivi karibuni imewaacha wafugaji
wakiwa masikini kwa baadhi ya Ng’ombe zilikamtwa na kuongeza kuwa kuna idadi ya
Ng’ombe zaidi ya 4,000 wamekamatwa katika eneo la Bukundi.
Aidha
Katibu huyo wa chama cha Wafugaji nchini aliendelea kusema kuwa jumla ya
Ng’ombe 1,089 wamepigwa Risasi huku wengine wakifa kwa njaa sambamba na
kukatwakatwa mapanga na kutoswa majini huku mbuzi na Kondoo wakiwa 315.
Hata
hivyo aliendelea kusema kuwa kwa upande wa mifugo iliyopotea alisema kuwa,
jumla ya Ng’ombe waliopotea katika operesheni hiyo wanafika 335 wakati nyumba
5,701 zikihofiwa kuchomwa moto na kuteketea.
Katibu
aliiomba Serikali kulifutilia kwa ukaribu suala hili watu walihusika waweze
kuwajibishwa na kuongeza kuwa kwa watu walioptelewa na mifugi ni bora
wakafidiwa kwani wanyama hao hawana makosa katika opereheni hiyo.
Mwisho.
No comments: