Na
Kahama
Febr 4, 2014.
JUSTINE KIMISHA MGENI MHALIKWA KWA TIKETI YA TADEA AKIHUTUBIA MKUTANO WA KAMPENI KATIKA KATA YA UBAGWE KUHUSU RUSHWA
MGOMBEA UDIWANI KWA TIKETI YA (TADEA )MAJINJA LUBIZA AKIHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KIJIJI CHA MAZILAYO KATA YA UBAGWE
KAMISHI WA ADC JUSTINE KIMISHA AKISISITIZA KUNUNULIWA KWA SHAHADA ZA WAPINGA KURA NI KUKOSA HAKI YAKO YA KATIBA
BAADHI YA VIONGOZI WAALIKWA KATIKA SIKU YA UZINDUZI WA KAMPENI YA UCHANGUZI WA UDIWANI WA KATA YA UBAGWE WILAYANI KAHAMA AMBAO HUNATALAJIWA KUFANYIKA SIKU YA TAREHE 9 ,2,2014 SIKU YA JUMAPILI
PIA BAADHI YA VIKUNDI VYA NGOMA BALI MBALI ZIKUWEPO KATIKA UZINDUZI HUO MWANA KWELA NA BAADHI YA WASANI
MH DIWANI MTARAJIWA AKIWA NA BAADHI YA VIONGOZI WA ADC KATIKA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KIJIJ CHA MAZILAYO KATA YA UBAGWE
BAADHI YA VIONGOZI WA TADEA WILAYA YA KAHAMA MKOANI SHINYANGA WAKIWA KATIKA MKUTANO WA UZIDUNZI WA KAMPENI YA CHAMA HICHO JANA
BAADHI YA WANANCHI WA KIJIJI CHA MAZILAYO KATA YA UBAGWE WAKISIKILIZA SERA ZA CHAMA CHA TADEA
WATAKIWA
KUTOCHAGUA DIWANI MBINAFSI NA MPENDA RUSHWA
WANANCHI wa Kata
ya Ubagwe Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wameaswa kutokuchagua Diwani ambaye
ni mbinafsi na Mpenda Rushwa katika harakati za uchaguzi mdogo unatarajiwa
kufanyika hivi karibuni katika kata hiyo kutokana na aliyekuwa Diwani
wake kufariki Dunia mwaka jana.
Hayo yalibainishwa
juzi na Katibu wa Chama cha TADEA Zakayo Kassana wakati wa uzinduzi wa Kampeni
za uchaguzi huo katika kijiji cha Mazirayo Kata ya Ubagwe Wilayani Kahama
ambapo kwa mwaka huu chama hicho kimeamua kumsimamisha Majinja Lubinza kugombea
kiti hicho.
Kassana alisema
kuwa kama Wananchi watamuweka Diwani ambaye atajali sana Maslahi yake na Rushwa
kwa ujumla basi watakuwa wamejimaliza wenyeye kwani viongozi kama hao kwa sasa
hawatakiwi kabisa katika jamii.
Aliwataka wananchi
wa kata hiyo kuchagua kiongozi mpenda maendeleo ambaye atafanya kazi kwa
maslahi ya Wanachi na sii chama anacotokea hali ambayo italeta chachu kubwa
katika kuhamisisha m aendeleo katika sehemu husika.
“kwa nini tusiwape
kipaumbel viongozi wanaopenda maendeleo?na chagueni mtu anayeweza kuwatumikia
na sii kuchagua mtu anayetokana na chama fualani inaweza kuja kuwagarimu hapo
siku za baadaye”Alisema katibu huyo wa chama cha TADEA.
Pia alitoa
angalizo kwa wananchi kutokuuza shahada zao kwani kufanya hivyo wanapoteza haki
yao ya kupiga kura na kusisiza kila mtu anapaswa kutunza shahada yake ili aweza
kupiga kura kuchagua kiongozi wake.
Katibu huyo
aliendelea kusisiza kuwa kwa kuchagua kiongozi anayeweza kutekeleza na
kusimamia misingi ya utawala bora pamoja na kutekeleza yale anayoagizwa
na Wananchi wake huyo ndio atakuwa kiongozi bora katika jamii inayomzunguka na
kuwataka kufanya maamuzi yalio sahihi.
Kwa upande wake
Mgombea Udiwani kwa tiketi ya chama cha TADEA Majija Libinza akiongea wananchi
wa Kijiji hicho alisema kuwa katika kipindi kichobaki ni kidogo cha uongozi na
kusema kuwa kama atapata ridhaa ya kuwaongoza wananchi hao atajitahidi katika
kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kilimo cha tumbaku ambacho
ni maarufu katika eneo hilo.
Uchaguzi katika
kata ya Ubagwe unatarajiwa kufanyika hivi karibuni kutokana na aliyekuwa
kiongozi katika kata hiyo Robert Mndula kufariki Dunia mwaka jana hali ambayo
imefanya uchaguzi katika kata hiyo urudiwe huku vyama vitatu vya CCM,
Chadema pamoja na TADEA vikionekana kuchuana vikali kupata kiticho.
mwisho
No comments: