sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » “KIKWETE AUNGWA MKONO UJENZI WA MAABARA SHINYANGA”

 mkuuu wa wilaya ya kahama Benson mpesya  mwenye sharti la drafit akiwa na waadishi wa habari katika ukaguzi wa mahabara katika shule ya sekondari Bugish kuona ujenzi huo.

 Dc mkuu wa wilaya ya kahama akitoa ufafanuzi juu ya ukamilishaji wa  ujenzi wa mahabara na waandishi wa habari kahama .
 Mtendaji wa kata ya nyasubi  Mussa isango akimuonyesha mkuu wa wilaya ya kahama Benson mpesya alijishika kiuno jinsi walipofikia katika Rita kwanye shule ya  sekondari ya nyasubi jinsi wanachi walipofikia na mchango wao katika ujenzi huo wa mahabara .

 Hivi ndiyo waandishi wa habari wilayani kahama walivyojitolea katika ujenzi wa mahabari katika shule za sekondari .

 Mkuu wa wilaya ya kahama Benson mpesya akiwanga  kokoto za zege .
 ukanguzi  wa mahabara katika shule ya sekondari ya nyasubi akiwa na waandishi wa habari .

 mkuu wa wilaya akiwa amebeba ndoo ya mawe katika kushiriki katika ujenzi wa  mahabara .
 waandishi wa habari wakipewa taarifa na mtendaji wa kata ya nyasubi mussa ishago
 muandishi wa gazeti la habarileo Raymond Mihayo akiwa katika moja ya ushiriki wa ujenzi wa mahabara katika shule ya nyasubi wilayani kahama.
 mkuu wa wilaya akipewa tarifa za ufatuaji wa matofari ambapo kambi hiyo imewekwa katika ofisi za halmashauri ya mji wa kahama ambapo jumla ya matofari elfu 31 ambayo yapo tayari kwa ajili ya kupelekwa katika shule mbalimbali wilayani hapo ambapo lengo ni kufikisha tofari elf 40.
 waandishi wa habari wakifanya kazi ya kuchota kokoto za ujenzi wa mahabara .
 mkuu wa wilaya ya kahama akichota kokoto
 Mwenyeki wa wandishi wa habari mkoa wa shinyanga shija
Felician katika shule ya sekondari ya bugisha

 Mkuu wa wilaya kahama Benson mpesya akiwanga kokoto ya kuwanga zege .

 Diwani ya kata ya mondo mh said akiangalia ufatuaji wa matofali
 waandisha habari wakimsiliza mkuu wa wilaya ya kahama juu wa ujenzi wa mahabari .
 Mtendaji wa kata ya nyasubi mussa ishago akiongea na waandishi wa habari juu ya ujenzi wa mahabara ktikati kata ya nyasubi.
 Hivi ndiyo ujenzi umefikia katika Rita shule ya sekondari nyasubi .
 Dc karibu sana mh diwani hayo ndiyo maneno ya dc mpesya kwa diwani wa kata ya mondo katika kumpongeza kwa kukamilishaji wake wa jengo la mahabara katika kata yake .
 Meona kazi yetu waandishi wa habari hayo ni maneno ya Dc mpesya
 Hapa ni kazi tu waandishi wa habari .
 Mkuu wa wilaya ya kahama akisitiza jambo la ujenzi wa mahabari kwa waandishi wa habari ofisini kwake .
 Mafundi wakiendelea na kazi .
 DC mpesya na waandishi wahabari pichani ofisini kwake.
 Mkuu haya ndiyo matofari Elf 31  ambapo fundi mkuu wa ufatuaji wa matofali juma ally alisema   kuwa lengo ni matofali Elf 40 ambapo tayari yapo ni Elf 31.
 Haya ndiyo matofari yalipo tayari kwa ujenzi huo wa mahabara .
Hapa ni kazi tu kwa waandishi wa habari .

Waandishi wa Habari Wilayani Kahama jana wameshiriki katika shughuli ya ujenzi wa vyumba vya maabara ya shule za sekondari katika azma ya kuunga mkono Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Waandishi  hao wa habari  walioongozwa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoaani humo (SPC) ,Shija Felician ,walikuwa bega kwa bega na  Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpesya  katika mradi  wa ujenzi  huo Shule ya Sekondari Nyasubi ,mjini Kahama jana.

Mwenyekiti huyo wa  SPC mkoani Shinyanga alimwambia mkuu huyo wa wilaya kuwa lengo la kushiriki ujenzi huo ni kumuunga mkono Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwani manufaa ya mpango huo ni makubwa kwa taifa na haupaswi kubezwa au kupuuuzwa na mtu yeyote wala chama chochote cha siasa.

“Taifa haliwezi kutegemea wanasayansi,wataalamu kutoka nje ya nchi hivyo lazima juhudi za lazima zifanywe kujenga maabara katika shule zote nchini,kuongeza vitabu vya masomo ya fizikia,kemia ,baolojia na hisabati ili maabara hizo zilete tija.”Alisema Felician.

Mpesya aliwashukuru wanahabari hao kwa kujitolea katika kufanikisha mpango huo kwa vitendo na kutaka wanajamii wengine kuiga mfano huo.

Naye Mkuu huyo wa wilaya alisema wameweza kufyatua matofali 31,000 hadi sasa kati ya lengo la matofali  41,000 kwa msaada wa wafanyabiashara,taasisi za umma na binafsi na migodi ya Dhahabu ya Buzwagi na Bulyankulu.

Alisema kazi ya ujenzi wa vyumba vya maabara katika halmashauri za Ushetu,Msalala na Mji wa Kahama inaendelea vizuri na anamatumaini ya kukamilisha kabla ya muda uliowekwa na Rais wa Jamhuri mjini Dodoma  mwaka jana na kusisitizwa tena hivi karibun.i

Kwa mfano alifafanua,Halmashauri ya Ushetu ilipanga kuwa na vyumba 45 vya maabara,katika hivyo 21 vimekaribia kukamilika na 20  vinaendelea kujengwa  na vinne katika hatua za mwisho.Halmashauri ya Msalala lengo ni vyumba 42,17 vimekamilika 23 vinajengwa na viwili vinatumika.

Halmashauri ya mji wa Kahama ,lengo ni vyumba 42,vitano vinafanya kazi, 37 viko katika hatua mbalimbali za ujenzi na vitakamilika kabla ya Novemba 30,mwaka huu.
Mratibu wa mradi huo Agnes Kahezela alifafanua kuwa baada ya kufyatuliwa matofali hayo hupelekwa moja kwa moja saiti kuendeleza shughuli za ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara za sekondari wilayani humo.

Mwisho 



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply