sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » HALMASHAURI YA MSALALA IMESIMAMISHA KAZI MRATIBU WA TASAF

Mkurungezi wa Halmashauri ya msalala SIMON Berege Akiongea na vyomba vya habari ofisini kwake juu ya shutuma za  Ubadilifu  mratibu wa tasaf 


Mkurungezi wa Halmashauri ya msalala  Simon Berege akiongea na waandishi wa habari 


KAHAMA .

HALMASHAURI  ya Msalala wilayani Kahama,imemsimamisha kazi mara moja Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF),Morris Oswago,baada ya kuwepo kwa kaya hewa 153, katika Mpango wa kunusuru kaya masikini ndani ya halmashauri hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Simon Berege,jana aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya kubaini kaya hizo hewa kupewa fedha za Mpango huo na kusababishia serikali hasara ya jumla ya shilingi milioni 30.076.

Berege alisema kuwa katika kufuatilia Mpango huo mapema mwezi huu,iligundulika kuwa baadhi ya kaya ziilingizwa katika mpango huo bila kuzingatia vigezo vilivyowekwa.


Akifafanua alisema kuwa katika kutekelezaji wa Mpango wa Tasaf awamu ya tatu,awali jumla ya kaya 58,137 zilitambuliwa kuwa ni masikini kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa kuzibaini.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply