sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » RC ATEKELEZA AHADI YAKE KUSAIDIA UJENZI WA SHULE. NA VITUO VYA AFYA MSALALA NA HALMASHAURI YA MJI


MKUU WA MKOA WA SHINYANGA ZAINAB TELLACK AKIKABIDHI MASUKA MWENYEKITI  WA HALMASHAURI YA MSALALA 

Mkuu wa mkoa akiangalia masuka yaliohadi kutoa katika vituo vya afya halmashauri ya msalala 

 Mwenyekiti wa halmashauri ya msalala  Mibako mabubu na Mkurungezi wa halmashauri ya msalala simon Berege wakipokea mashuka toka kwa mkuu wa Mkoa wa shinyanga 

 Mashuka ya msaada  katika vituo vya afya msalala 

Mkuu wa mkoa wa shinyanga Zainab Tellack

 SERIAKALI mkoani Shinyanga imetimiza ahadi yake juu ya ujenzi wa shule ya msingi Mhungula iliyopo katika Kata hiyo Halmashauri ya mji wa Kahama.

Akikabidhi mabati hayo zaidi  140  yaliyotolewa na mkuu wa Mkoa huo Zainab Tellack, kwa mkurugenzi mtendaji wa halamsahauri hiyo Anderson Msumba, Diwani wa Kata ya Mhungula  Ignas Shabani  alimwambia mkurugenzi huyo kuwa mkuu wa Mkoa huo aliahidi kusaidia ujenzi huo.

Aidha Diwani Shabani alieleza kuwa mabati hayo yamegawanywa kwa shule mbili za Kata hiyo ambapo shule ya msingi Mhungula imepatiwa mabati 90 huku shule ya msingi Bukondamoyo nayo  ikipatiwa mabati 57.

Akifafanua zaidi Diwani  alisema licha ya kuipongeza serikali kwa msaada huo lakini bado kuna changamoto zingine zinazoikabili Kata ya Mhungula likiwemo suala la umeme,maji pamoja na miundo mbinu za barabaraba ambazo hazijatatuliwa.

Akipokea msaada wa mabati uliotolewa na mkuu huyo wa Mkoa kutoka kwa Diwani huyo mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Anderson Msumba alimshukuru mkuu huyo wa Mkoa kwa msaada wake.

Msumba alisema kuwa licha ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kufanya ziara yake katika shule hiyo na kubaini changamoto hizo na Halmashauri ilikuwa tayari imejipanga vyema katika kukabiliana na changamoto hizo ambapo alidai kwamba kabla ya mkuu wa Mkoa kufika shuleni halmashauri ilitenga kiasi cha shilingi milioni192 kwaajili ya ukarabati wa vyumba vya madarasa hivyo mchango wake utasaidia kuzidi kuboresha.

Mwisho



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply