John Magufuli ameagiza Sh 200
milioni zilizopangwa kutumika katika mradi wa maji katika kambi ya jeshi zianze
kuimarisha miradi ya maji kwa wananchi kwanza.
Akizungumza leo, Alhamisi Julai
20 katika ziara yake akiwa ameambatana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza,
Magufuli amesema amebaini kuwa pampu za maji wilayani Ngara zimeharibika kwa
zaidi ya wiki tatu na kuwa wilaya hiyo ina uhaba mkubwa wa maji.
Alimuita, Mhandisi wa Maji
ajieleze ni kwa nini pampu hizo hazifanyi kazi na baada ya kumsikiliza ndipo
alipofanya uamuzi huo.
Akifafanua kuhusu hali ya maji,
mhandisi huyo amesema awali visima vya maji wilayani hapo vilikuwa vikihudumia
watu 400 lakini kwa sasa wilaya hiyo ina watu zaidi ya 240,000 na hivyo visima
hivyo havitoshelezi.
“Tulikuwa tuna idadi ndogo ya
watu sasa hivi imeongezeka, lakini tangu pampu iharibike, tumetengeneza mbili
na kisima kimoja hakina pampu,” amesema.
Baada ya mhandisi huyo kufafanua
hayo ndipo Rais alimuita Mkurugenzi wa Halmashauri kueleza mipango yake, ndipo
Mkurugenzi huyo aliposema mradi wa maji wa Sh 200 milioni utaanza kwanza katika
kambi ya jeshi.
Kauli hiyo ndiyo iliyomfanya Rais
Magufuli kushauri fedha hizo zitumike katika miradi ya maji katika makazi ya
wananchi kwanza.
“Wanajeshi wapo 200 na wananchi wapo zaidi ya 20,000 sasa si
bora waanze wananchi kwanza,” amesema.
|
No comments: