Mfano wa mabomu ambayo yamekamatwa kutoka kwa kijana huyo.
JAMANI! Siku chache tu kufuatia Jeshi la Polisi Tanzania kupitia msemaji
wake, Advera Bulimba kupiga marufuku maandamano na mikusanyiko ya
kisiasa nchini kote kwa hofu ya kutokea kwa uvunjifu wa amani, kijana
mmoja (jina halikupatikana mara moja) anashikiliwa na Jeshi la Polisi
Mkoa wa Shinyanga kwa madai ya kunaswa na mabomu 10 kinyume cha sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Justus Kamugisha.
ILIKUWA SAFARI YA DAR
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha ndani ya jeshi hilo mkoani Shinyanga,
kijana huyo ambaye pia ni mfanyabiashara wa madini, alikamatwa usiku wa
Novemba 5, mwaka huu nyumbani kwa baba yake mzazi mjini Kahama ikidaiwa
kwamba alikuwa katika mchakato wa safiri ya jijini Dar na mabomu hayo.
CHANZO NI RAIA WEMA
“Polisi walipewa taarifa na raia wema Wakaenda nyumbani kwa baba yake
ambako kweli walimnasa akiwa na mabomu hayo kumi.
Hii hali imezua
maswali mengi! Baadhi ya watu wanahisi Dar ilikuwa kituo cha kupita tu,
huenda alikuwa akienda nje ya nchi, wengine wanasema Dar ndiyo kilikuwa
kituo chake kikuu.
“Lakini walimkamata, wakampeleka polisi na mabomu yake yote. Unajua
hakuna kipindi ambacho Jeshi la Polisi Tanzania liko macho kama sasa.
Lengo kubwa ni kulinda amani ya nchi, hususan baada ya uchaguzi mkuu
kupita ambapo baadhi ya watu walionesha ishara ya kutaka kuvunja amani
na kuleta vurugu,” kilisema chanzo hicho.
DCI Diwani.
Kufuatia tukio hilo, baadhi ya wananchi mjini Kahama wamelitaka jeshi la
polisi kuzidisha ulinzi na upelelezi ili kuwabaini watu wanaoweza
kumiliki zana za kijeshi kinyume cha sheria hasa katika kipindi hiki
ambacho, nchi imekuwa katika mapito ya uchaguzi.
“Kwa sasa jeshi la polisi si la hapa Kahama au Shinyanga tu, nchi nzima lazima liwe makini sana.
Kuna watu wanataka kuvunja amani. Lakini kuna watu tunapenda amani,” alisema Chubwa Pomongo, mkazi wa Kahama.
lilimsaka Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Shinyanga, SACP Justus Kamugisha na kumuuliza kuwepo kwa madai ya kijana
huyo kukamatwa ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli. Alhamisi iliyopita, majira ya usiku hivi, Jeshi la Polisi
Mkoa wa Shinyanga lilimkamata huyo mtu akiwa na mabomu kumi (10) na
ditoneta (za kusababisha mlipuko) elfu tano (5,000).
“Mtu huyo anajishughulisha na biashara ya madini katika mgodi mdogo wa
Ilalo, Geita.
Bado tunamshikilia kwa vile uchunguzi unaendelea ili kujua
lengo la yeye kuwa na mabomu hayo kumi na ditoneta elfu tano ni nini.”
Kamanda Kamugisha alipoulizwa jina la mtuhumiwa huyo, alisema mpaka
afike ofisini kwake kwa vile alikuwa nje ya ofisi kwa siku hiyo ya
Jumamosi.
DCI DIWANI
Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Tanzania (DCI),
Diwani Athuman Msuya kwa lengo la kusikia kauli yake kuhusiana na tukio
hilo lakini simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
TUJIKUMBUSHE
Mwishoni mwa wiki iliyopita jeshi la polisi nchini lilipiga marufuku
ombi la maandamano la baadhi ya vyama vya siasa nchini baada ya
uchunguzi wake kubaini kuwepo na mihemko ya kisiasa ndani ya jamii
inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani.
Kutokana na hali hiyo, jeshi hilo lilisema litaendelea kushikilia
msimamo wake wa awali wa kuzuia mikutano na maandamano yoyote mpaka hali
itakapotengemaa.
Kauli ya jeshi hilo imefuatia baada ya baadhi ya vyama vya siasa
kuwasilisha ombi la kufanya mikutano ya hadhara na maandamano nchi nzima
huku vyama vingine vikitaka kufanya maandamano yasiyo na ukomo.
Kufuatia hali hiyo jeshi hilo limewataka wananchi kushirikiana na jeshi
la polisi ili kudhibiti hali hiyo huku likivitaka vyama vya siasa
kufuata sheria na kutii ili kuepusha vurugu zisizo na ulazima.