Mgombea
urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk Mohamed Shein na mwenzake wa ya
CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad jana walikutana kwa faragha kwa takriban
saa tano, lakini hakuna taarifa iliyotolewa kuhusu kilichojadiliwa
kwenye kikao hicho.
Kikao
hicho, ambacho pia kiliwahusisha marais wastaafu wa Zanzibar na Jamhuri
ya Muungano, Ali Hassan Mwinyi na Amani Karume, kimefanyika katika
kipindi ambacho kuna hali ya sintofahamu visiwani hapa tangu Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha atangaze kufuta
matokeo ya uchaguzi wa Rais na wawakilishi.
Jecha,
ambaye alifuta matokeo hayo siku chache baada ya Maalim Seif
kujitangazia ushindi, aliahidi kuitisha uchaguzi mpya ndani ya siku 90,
lakini CUF imesema haitashiriki.
Kikao kilichofanyika Ikulu ya Mnazi Mmoja mjini hapa, kilianza saa 4.15 asubuhi na kumalizika saa 9.40 mchana.
“Ikulu
ilikuwa tulivu hakuna kilichoonekana kuongeza harakati licha ya vizuizi
vya kamba vilivyokuwa vimezungushwa tangu ulipomalizika uchaguzi,”
alisema mmoja wa maofisa watendaji wa ofisi hiyo ya Rais.
Hii
si mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu kumalizika kwa uchaguzi
ulioiweka Zanzibar njia panda baada ya ZEC kuamua kutoendelea kutangaza
matokeo.
Hata
hivyo, inaonekana ni mara ya kwanza kwa wagombea hao kukaa meza moja na
safu kubwa ya viongozi hao wa kisiasa na maongezi yao kuchukua muda
mrefu.
Mkutano
huo umefanyika siku moja baada ya Maalim Seif kukutana na watendaji wa
kamati za utendaji za matawi na wilaya wa Unguja na pia jana kuongea na
viongozi wa ngazi hizo kwa upande wa Pemba.
Katika vikao hivyo, Maalim Seif amekuwa akisisitiza wafuasi kuendelea kuwa watulivu huku akiahidi ku
No comments: