sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » UCHAGUZI MKUU ZANZIMBAR DK SHEIN NA MAALIMU SEIF WAKUTANA FARAGHA IKULU

Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk Mohamed Shein na mwenzake wa ya CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad jana walikutana kwa faragha kwa takriban saa tano, lakini hakuna taarifa iliyotolewa kuhusu kilichojadiliwa kwenye kikao hicho.
 
Kikao hicho, ambacho pia kiliwahusisha marais wastaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano, Ali Hassan Mwinyi na Amani Karume, kimefanyika katika kipindi ambacho kuna hali ya sintofahamu visiwani hapa tangu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha atangaze kufuta matokeo ya uchaguzi wa Rais na wawakilishi.
 
Jecha, ambaye alifuta matokeo hayo siku chache baada ya Maalim Seif kujitangazia ushindi, aliahidi kuitisha uchaguzi mpya ndani ya siku 90, lakini CUF imesema haitashiriki.
 
Kikao kilichofanyika Ikulu ya Mnazi Mmoja mjini hapa, kilianza saa 4.15 asubuhi na kumalizika saa 9.40 mchana.
 
“Ikulu ilikuwa tulivu hakuna kilichoonekana kuongeza harakati licha ya vizuizi vya kamba vilivyokuwa vimezungushwa tangu ulipomalizika uchaguzi,” alisema mmoja wa maofisa watendaji wa ofisi hiyo ya Rais.
 
Hii si mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu kumalizika kwa uchaguzi ulioiweka Zanzibar njia panda baada ya ZEC kuamua kutoendelea kutangaza matokeo.
 
Hata hivyo, inaonekana ni mara ya kwanza kwa wagombea hao kukaa meza moja na safu kubwa ya viongozi hao wa kisiasa na maongezi yao kuchukua muda mrefu.
 
Mkutano huo umefanyika siku moja baada ya Maalim Seif kukutana na watendaji wa kamati za utendaji za matawi na wilaya wa Unguja na pia jana kuongea na viongozi wa ngazi hizo kwa upande wa Pemba.
 
Katika vikao hivyo, Maalim Seif amekuwa akisisitiza wafuasi kuendelea kuwa watulivu huku akiahidi ku

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply