sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » DC KAHAMA APINGA WIZI WA MITIHANI NI UVUMI TU WAKUHARIBU TASWILA YA ELIMU KAHAMA

 Moja ya shule za wilayani kahama ambazo zipo kwenye ubora wa kupandisha  Elimu.
 Walimu wa shule ya msingi mwakata wilayani kahama wakiwapatia wanafunzi kifungua kinywa uji
Baadhi ya wanafunzi wakinywa uji shule ili kupata mawanzo mazuri wakiwapo darasa
KAHAMA

SERIKALI wilayani Kahama,imepinga madai ya baadhi ya walimu wa Sekondari kushikiliwa na polisi kwa kuhusika na kukutwa na majibu ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne, kuwa ni uvumi uliolenga kuharibu taswira ya elimu ya wilayani humo.

Akiongea na waandishi wa Habari,Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Vita Kawawa, alisema baada ya kuulizwa na waandishi wa Habari,alitumia vyombo vyake vya ulinzi na usalama vya wilaya na kubaini katika Halmashauri tatu zilizomo wilayani mwake hakuna tukio lolote la kuibiwa kwa mitihani ya Taifa ya Kidato cha nne.


Kauli hiyo ilikuja baada ya kuwepo kwa utata kwenye tukio hilo,ambalo kwa mujibu wa baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vilimnukuu aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga,akidai polisi wilayani Kahama inawashikilia kwa uchunguzi walimu wawili kati ya 12 wa shule ya sekondari ya Anderlek Ridgers wanaodaiwa kukutwa na majibu ya mtihani wa somo la historia.

Kawawa alisema baada ya kupata taarifa hizo dhidi ya walimu wa shule hiyo alianza kufuatilia kwa makini tuhuma hiyo na kubaini kuwa ni uvumi wala hapakuwa na walimu waliosimamia mitihani kukutwa wameiba ama wanafunzi wahitimu kuingia katika vyumba vya mitihani wakiwa tayari majibu ya somo lolote katika wilaya ya Kahama.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply