sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » MBUNGE KUIBULUZA HALMASHAURI YA MJI NZEGA MAHAKAMANI



Na
     Nzega
January 9,2014,

 MBUNGE KUIBULUZA H/M MAHAKAMANI.

KATIKA  Hali isiyo ya kawaida mbunge wa Jimbo la Nzega Dkt,Hamis Kigwangalla ameongoza maandamano na wananchi zaidi ya 2000 wilayani Nzega ya kupinga maamuzi ya Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya kwa matumizi ya Fedha za Ushuru wa Huduma kutoka mgodi wa dhahabu wa Resolute Bill 2.1.

Akihutubia mamia ya wananchi katika viwanja vya maengesho ya magari  akiwa ameambatana na madiwana watano wanao muunga mkono alisema kuwa amepanga kuweka zuio la matumizi ya fedha hizo katika mahakama Kuu ili suala hilo liweze kupatiwa ufumbuzi wa msingi.

Alisema Halmashauri hiyo itafikishwa mahakamani ili iweze kuzuiwa kupanga matumizi na maadhiumio ya Baraza hilo ambalo aliliita lenye madiwani mizigo ambao hawana uwezo wa kupambanua mambo ya msingi dhidi ya wananchi wao.

Hatua hiyo imetokea baada ya Baraza la madiwani kuidhinisha fedha hizo zitumike katika kukamilisha miradi na kuibua miradi ya maendeleo ya wananchi kwa kila kata huku wasimamizi wa kuu wa miradi hiyo na kuibua kwa kushirikiana na wananchi wakiwa ni madiwani.

Baraza hilo lilithia kwa kupiga kura za ndio 34 huku kura za madiwani ambao hawakuridhia na matumizi hayo ya pesa wakiwa 5 pamoja na mbunge huyo hali ilipelekea Mbunge kutoka kikaoni.

Akiwahutubia wananchi Kigwangalla alisema kuwa fedha hizo za ushuru wa huduma kutoka Resolute zikipelekwa kwenye miradi  kwa kila kata zitatafunwa na baadhi ya madiwani ambao hawana nidham ya fedha na kuongeza kuwa fedha hizo hazita leta tija na matokea sahihi kwa kukidhi kero za wananchi.

Mbunge huyo aliwaambia wananchi hao kuwa vita hiyo anayo pigwa ni vita inayoanzia ndani ya chama cha mapinduzi huku lawama kubwa akimtuhumu katibu wa chama cha mapinduzi CCM kajoro vyohoroka kwa kuendesha mchakato wa kuwashinikiza madiwani kugawana fedha hizo kwa kila kata.

Alisema kuwa hatofika katika ofisi ya chama hicho hadi pale katibu huyo wa chama atakapo hamishwa na kuongeza kuwa hatofika katika ofisi za Halmashauri ya wilaya m,paka matumizi ya fedha hizo yabadilishwe.

Vipaumbele vya mbunge huyo dhidi ya fedha hizo ni ununuzi wa mitambo ya ujenzi wa Barabara vijijini ilikukidhi haja za wananchi,ununuzi wa mtambo wa kuchimbia visima ilikukidhi kero ya maji pamoja na kuanzisha Benk ya kijamii itakayo weza kukopesha wajasilia mali.

Alisema kuwa mapendekezo hayo yalipitishwa toka vikao vya awari laikini baraza hilo lilipindisha kanuni za baraza na kulazimisha kutoa maadhimio ya awari bila kufuata taratibu na kanuni.

Mbunge huyo aliwaita madiwani wote waliopiga kura za pesa hizo zipelekwe kwenye miradi ya kata zao kuwa ni madiwani mizigo katika Halmashauri zao na kuahidi kuwaambia wananchi wao dhidi ya uzaifu wa hoja zao.

Awari ya hapo Diwani wa kata Nzega Mjini Domick clement kizwa kupitia CUF alimpongeza mbunge huyo na kuwa pongeza madiwani wa CCM walio muunga mkono mbunge huyo dhidi ya kupinga matumizi ya fedha hizo.

Mbunge huyo aliongoza maadamano hadi ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Nzega huku wananchi wakiwa wamebeba ujumbe mbalimbali dhidi ya fedha hizo na kuitaka serikali kusimamisha haraka matumizi ya pesa hizo badala yake wafuate matakwa ya msingi yenye kutatua kero za wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Nzega Bituni Msangi akipokea maandamano hayo na kuyajibu alisema kuwa ombi la wananchi hao limepokelewa na ofisi yake na kuwaahidi kuyafanyia kazi huku akiomba utulivu na amani idumu kwani suala hilo linafanyiwa kazi.

Mwisho.




«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply