Na
Mkurungezi wa halmashauri ya ushetu isabela chilumba akitoa tangazo katika ukumbi wa maarifa ya jamii ya kuwataka waandishi wa habari kuwacha vifaa vya kazi katika paty kama vile kamera na kamera za mnato
Kahama
Jan
14, 2014.
Katika
hali ya kushangaza mkurungezi wa halmashauri ya ushetu wilayani kahama Isabela
chilumba aangusha bonge la sherehe kwa lengo la kuwashawishi madiwani wa halmashauri yake kupitisha
makisio ya bajeti ya kiasi cha bilioni 32.5mwaka 2014/2015.
Katika
sherehe hiyo ambapo vyombo vya habari havikurusiwa kuingia na vifaa vya
kufanyia kazi vikiwemo kamera na vifaa
vingine vya kurekondia sauti kwa madai ya kuwa kilikuwa ni kubadilishana
mawanzo Baina ya wakuu wa idara ,madiwani na kamati ya ulinzi na usalama ya
wilaya ya kaham,
“Hata
nyinyi waandishi tunawaalika katika Sherehe hiyo muhudhurie lakini msije mkaja
na vifaa ya kufanyia kazi zenu kama kamera na vyombo vya kurekodia sauti hii ni
shrehe ya kubadilishana na mawazo tuu”, Alisema Isabela Chilumba Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Ushetu.
Hata
hivyo Mwandishi wa Gazeti la Nipashe alifanikiwa kuingia katika sherehe na
kufanikiwa kuona baadhi ya Madiwani wakiwa katika makundi makundi wakijadili
baadhi ya mambo ambayo iliashiria kuna baadhi ya mambo yalikuwa yakipangwa
katika sherehe hiyo yalioashiria dalili za Rushwa kutoka Mkurugenzi huyo ili
waweze kupitisha bajeti.
Halmashauri
hiyo ya Wilaya ya Ushetu katika kikao
cha baraza la Madiwani kilichofanyika muda mchache kabla ya shrehe hiyo ilipanga
kupitisha makisio ya kutumia kiasi cha
shilingi Bilioni 32.5 katika bajeti ya kipindi cha mwaka 2014/2015 kwa
ajili ya Mishahara kwa wafanyakazi na miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Ushetu Isabela
Chilumba alisema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya matumuizi ya kawaida na miradi
mbalimbali ya maendeleo.
Alisema
kuwa katika bajeti hiyo shilingi bilioni 30.7 ni ruzuku kutoka Serikali kuu
ikiwa ni sambamba na wahisani mbalimbali ambapo ni sawa na punguzo la asilimia
11 ikilinganishwa na mwaka 2013/2014 ambapo makisio ilikuwa ni kiasi cha
shilingi bilioni 39.3 ikiwa bilioni 37 ni ruzuku kutoka serikalini.
Chilumba
aliendelea kusema kuwa katika bajeti ya mapato ya ndani Halmashauri yake imekisia
kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kutoka katika vyanzo mbalimbali
vya mapato ya ndani sawa na punguzo la silimia 21 ikilinganishwa na mwaka
uliopita.
Ailisema
kuwa baadhi ya vipaumbele katika bajeti hiyo ni pamoja na suala la Elimu, Afya
na maji pamoja na miundombinu ya barabara pamoja na ujenzi wa Hospitali mpya ya
Wilaya ya Ushetu ambayo kwa sasa haipo.
Mkurugenzi
huyo aliendelea kusema kuwa katika mapato ya ndani ya Halamshauri ya Ushetu kwa
kiasi kikubwa yanatokana na zao la Tumbaku ambalo kwa kipindi cha mwaka
2013/2014 makisio ya zao hilo yalikuwa ni shilingi milioni 863.9 ambapo
katika makusanyo Halmashauri hiyo ilipata kiasi cha shilingi bilioni 1.02 sawa
na ongezeko la asilimia 118 ikiwa shilingi milioni 157.7
Hata
hivyo katika uwasilishwaji wa makisio ya bajeti hiyo maadhi ya Madiwani wa
Halmashauri waliishauri serikali kuangalia uwezekano wa kutotegemea sana ushuru
wa zao la Tumbaku ambao ndio mkubwa kutokana na zao hilo kwa sasa kuwa katika
wakati mgumu wa kupigwa vita.
“Tunaweza
sisi kama Halmashauri kutafuta zao lingine mbadala la kuiingizia Halmashauri
yetu mapato badala ya zao la Tumbaku ambalo siku likipigwa marufuku basi mapato
yote yatakosekana na hivyo halmashauri kushindwa kujiendesha”,Dowa Makingi
Diwani wa Kata ya Nyankende.
mwisho
No comments: