sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » TRA KAHAMA YAWATOLEWA UVIVU WAFANYABISHARA WANAOGOMA KULIPA KODI



Na 
Kahama
Jan 13, 2013.


MAMLAKA ya Mapato (TRA) Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imesema kuwa haitasita kuwachukulia hatua wafanyabiasha ambao watakwepa kulipa mapato kwa mamlaka hiyo kwa mujibu wa sheria na taratibu zinavyosema.

Hayo yalisemwa juzi na Meneja wa Mamlaka hiyo Wilyani Kahama Peter Nkwabi wakati akiongea na Gazeti la nipashe  juu ya baadhi ya wafanyabiashara Wilayani hapa kuwa chanzo cha kupoteza mapato kwa mamlaka hiyo kwa kukwepa kulipa kodi.

Nkwabi alisema kuwa kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi huku wakisingizia kuwa biashara zao bado ndogo hali ambayo hawapaswi kulipa kodi katika mamlaka hiyo.

“Wafanyabiashara wengi hasa katika Mji wa Kahama wanahisi kuwa suala la kulipa kodi katika mamlaka hiyo siyo halali na kuwa wanasema uongo wanapoulizwa juu ya kiasi cha fedha wanazingiza kwa siku na kuipa mamlaka wakati mgumu katika kuwakadiria juu ya mapato yao wanayoingiza”, Alisema Peter Nkwabi.

“Kwa  mujibu wa sheria za TRA maafisa wake wanatakiwa kukaa katika kila duka kuangalia mfanyabiashara anauza kiasi gani kwa siku lakini wafanyabiashara hawa wamekuwa wagumu kukaguliwa na ndio maana wanakuwa wakilalamika kwa kitu wasichokijua”, Aliongeza Meneja huyo wa TRA Peter Nkwabi.

 Nkwabi alisema kwa sasa wao kama mamlaka hawatakubali kuona mamlaka hiyo inakosa mapato kwani tumeazimia kwa wale wote watakaokwepa kulipa mapatao ya Serikali tutawachulia hatua kwa mujibu wa sheria za Mamlaka husika zinavyosema

Aidha aliendelea kusema kuwa unakuta mfanyabiashara unakudanganya juu ya mapato yake kwa siku na kuongeza kuwa mara nyingine tunakuta magari makubwa yakishusha mizigo mikubwa na kutufanya tuyakubali makadirio yake.

Kwa upande wao baadhi ya Wafanyabiashara mjini Kahama walitoa malalamiko yao juu ya TRA kwa kusema kuwa maafisa wa Mamlaka hiyo wamekuwa wakiwalazimisha kufungua droo zao na kuhesabu fedha ili wajue juu ya mauzo yao kwa siku.

Pia walikataa kutumia mashine za (EFD ) mpya za mamlaka hiyo kwa kusema kuwa wao hawawezi kuzitumia kwani elimu yao bado ni ndogo ya kutumia mashine hizo huku wakitoa visingizio vya kukatikakatika kwa umeme mara kwa mara kutawaathiri katika biashara zao.

Wafanyabishara hao waliazimia kuitisha mkutano mwingine hivi karibuni kwa lengo la kujadili mambo hayo ikiwa ni sambamba na kutoa maamuzi juu ya kumkataa mwenyekiti wa chemba ya wafanyabisha Mkuu wa Wilaya mstaafu Meja Bahati Matala kwa kudai kuwa hawawezi kuongozwa na mtu ambaye sii mfanyabiasha.

 Mwisho




«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply