Shinyanga
Febr 24
Meneja wa mgodi wa Buzwagi philbert Rweyemamu akitoa maada kwa wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga kwenye mkutano kushoto ni mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Rufunga .Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa shinyanga All Rufunga katika mkutano wa wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga na migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu kwa kuwapatia fursa ya kufanya nao biashara .
Afisa mahusiano wa maendeleo ya jamii wa mgodi wa buzwagi Stephen kisakye hakiteta jambo na mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Rufunga wakati wa mkutano na wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga juu ya kufanya biashara na migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu .
Meneja wa Royal supermarket2008 William Matonange akitao maada juu ya kufanyabiashara na makampuni makubwa ya migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu na wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga.
Mwenye miwani ni Afisa maendeleo ya jamii wa migodi wa Bulyanhulu Abdahall mssika wakisikiliza maada mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga
Afisa maendeleo ya jamii mwenye tai moses msofe akiongea na katibu wa wafanyabiashara mkoa wa shinyanga juu ya kufanya shughuli na migodi hiyo ya Africa Barrick gold mine
Baadhi ya wafanyabiashara wakisikiliza mada mbali mbali juu ya kufanyabiashara na migodi
Meneja wa Royal supermarket2008 William matonange wakiteta jambo na mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Nassor Rufunga kabla ya kuanza mkutano na wafanyabiashara
Afisa maendeleo ya jamii wa mgodi wa Bulyanhulu Abdahal mssika akimkaribisha mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Nassor Rufunga kabla ya kuanza mkutano na wafanyabiashara na migodi ya Africa Barrick gold mine mjini shinyanga
Afisa mahusiano wa Buzwagi Blandina munghezi Akisikiliza mada mbalimbali zinazotolewa na wafanyabishara kwenye mkutano huo na migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu mjini shinyanga
Mwenye suti kijivu na karatasi mkononi meneja wa maendeleo ya jamii wa mgodi wa Buzwagi Stephen kisakye akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa shinyanga Ally Nassor Rufunga kabla ya kuanza kwa mkutano na wafanyabiashara wa mkoa wa shinyanga .
KUENDESHA Biashara bila ya kufuata misingi ya Sheria, taratibu na
kiwango cha juu cha maadili ni moja kati ya Changamoto zinazowakabili
Wafanyabiashara Mkoani Shinyanga kupata fursa ya kufanya biashara na Migodi ya
Barrick Tanzania.
Hayo yalisemwa juzi na Afisa kutoka katika kitengo cha Ugavi katika
Migodi ya Afrikani Barrick gold Mine Dickson Liwumba katika kikao kilichowajumuisha
Wafanyabiashara waliopo Mkoani Shinyanga na wale wanaofanya kazi na Migodi hiyo
kutoka sehemu mbalimbali kanda ya ziwa.
Liwumba alisema kuwa mbali na Changamoto hiyo pia Wafanyabiashara wa
Mkoa wa Shinyanga wamekuwa hawapati fursa hizo pia kutokana na bidhaa zao
kutokuwa na kiwango na kutomudu idadi ya vitu vinavyohitajika kwa wawekezaji
hao.
Afisa huyo alisema kuwa pia ushirikiano baina ya Wafanyabiashara wa
Mkoa wa Shinyanga na kutoridhika pia katika suala zima la kujiendeleza nalo ni
tatizo kubwa hali ambayo inakuwa vigumu hata kuomba Zabuni katika makapuni hayo
pindi zinapotokea.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga akifungua
mkutano huo uliandaliwa na Kampuni ya African Barrick Gold Mine alisema kuwa
Wafanyabiashara hasa wa Mkoa wa Shinyanga wanapaswa kujua kuwa wao bado wana
fursa kubwa ya kufanya kazi na migodi hiyo miwili.
Alisema kuwa anawashukuru pia Uongozi wa Migodi hiyo miwili ya Buzwagi
na Bulyanhulu kwa kufanya mkutano na kutoa Elimu kwa Wafanyabiashara hasa wa
Mkoa wa Shinyanga katika kufuata Sheria na muda katika kuendesha biashara zao
hasa katika maeneo ya wawekezaji wa Migodi.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Shinyanga alisema kuwa Wawekezaji wanataka bidhaa
zenye kiwango na kuongeza kuwa kwa kutumia Mkutano huo Wafanyabiashara wa Mkoa
waShinyanga hawana budi kubadilika na kuongeza kuwa kama kuna masuala ya
kiserikali yanayowasumbua basi ofisi yake ipo wazi kwa kutoa kutoa ushauri wa
kibishara.
Pia Rufunga aliwaomba Kampuni hiyo kuwa na utaratibu wa kuendesha mikutano
kama hiyo mara kwa mara kwa lengo la kutoa Elimu kwa Wafanyabiashara hao hali
ambayo inaweza kuleta mabadiliko hasa kwa Wafanyabiashara wa Mkoa wa Shinyanga
kuweza kuchangamkia fursa zilizopo katika migodi inayowazunguka.
Mkutano huo wa siku moja uliofanyika mjini Shinyanga ulijumuisha
Wafanyabiashara kutoka Mkoa wa Shinyanga na wale ambao tayari walishaanza
kufanya biashara na kampuni hiyo huku lengo kubwa likiwa ni kutoa Elimu kuhusu
kuweza kupata fursa za kufanya biashara na Kampuni ya Barrick
mwisho
No comments: