Na Mohab Dominick
Baadhi ya wachimbaji wadogo katika lashi ya nyangalata wilayani kahama mkoa shinyanga
wachimbaji wadogo wakiosha mchanga hunaosadikiwa kuwa na dhahabu katika kijiji cha nyangalata wilayani kahama mkoani shinyanga
Kahama
Febr
28,2014.
WATENDAJI
WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI WATAKIWA KUTOKAA MAOFISINI
WATENDAJI
wa Wizara ya Niashati na Madini waliopewa Dhamana ya kusimamia sheria za
Wachimbaji wadogo hapa Nchini wametakiwa kutokaa maofisini badala yake
wazunguke kwa wachimbaji wadogo kwa
madhumuni ya kutoa Elimu kwao juu uchimbaji wa kufuata sheria.
Hayo
yalisemwa juzi na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji wadogo Mkoa wa
Shinyanga Nicodemus Majambe wakati akiongea na Mwandishi wa habari hizi juu ya
vikwazo wanavyovipata Wachimbaji wadogo hapa nchini katika kupata maeneo ya
Uchimbaji.
Majabe
alisema kuwa Wachimnbaji wadogo hawana Elimu juu ya kupata maeneo ya uchimbaji
wa Madini na kuongeza kuwa kama maoafisa wa Madini wasingekaaa maofisini basi
kusingekuwa na migogoro yeyote juu ya kupata maeneo ya Uchimbaji.
Alisema
kuwa katika meneo ya Uchimbaji wa Madini Wakuu wa Wilaya wamekuwa wakipta kazi
ya kutoaa Elimu ya uchimbaji katika maeneo hayo kazi ambayo ilitakiwa kutolewa
na maoafisa wa Madini wa Sehemu husika.
Makamu
Mwenyekiti huyo alisema kuwa katika Mkutano waliokaa na Waziri wa Niashati na
Madini Mjini Dodoma walikubali kuwa na ushirikiano mkubwa baina ya Viongozi wa
Wachimbaji wadogo na Watendaji wa Wizara ya madini kwa ujumla.
Pia
alisema kuwa urasimu uliopo kati ya Watendaji wa Wizara ya Madini na Nishati
Tanzania ndio unaosababisha kuwepo migogoro mingi baina ya Wachimbaji wadogo na
Makampuni makubwa ya uchimbaji.
“Kuna
kesi nyingi ambazo zipo baina ya
Wachimbaji wadogo na Makampuni makubwa ya uwekezaji zinazosababishwa na watendaji wa Wizara hiyo
katika sehemu mbalimbali hapa nchini Waziri Mwenye dhamana na kuwa hana taarifa
juu Migogoro hiyo ambayo inaleta mvutano mkubwa baina yapande hizo
mbili”, Alisema Nicodemus Majabe.
Aidha
alisema kuwa baadhi ya migogoro hiyo ni pale wachimbaji wadogo wanapoomba leseni
za maeneo ya kuchimba lakini wamekuwa
wakipewa maeneo tofauti na y ale waliomba huku yale ya awali wakipewa
wawekezaji wenye uwezo.
“Kuna
maeneo kama yale ya Ny’angwale, Mwazimba, Kishapu na Mengine mengi katika
Wilaya ya Kahama amabayo yaliombwa na Wachimbaji wadogo kwa ajili ya kufanya
shughuli za uchimbaji lakini maeneo hayo walipewa wawekezaji wakubwa”,
Alisisitiza Makamu Mwenyekiti huyo.
Makamu
Mwenyekiti huyo alimuomba Naibu Waziri anayehusika na kitengo cha Madini
Stephen Masele kujitahidi katika kuondoa migogoro hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa
imekuwa ni kero kwa Wachimbaji wadogo na Wawekezaji wa migodi na Serikali kwa
ujumla.
mwisho
No comments: