sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » SERIKALI KUWEKA MFUKO MAALUM WA KUENDELEZA KILIMO CHA ZAO LA PAMBA



Na  Mohab Dominick
Kahama
March 9, 2014.

SERIKALI imeshauriwa kuweka mfuko maalum kwa ajili ya kuendeleza Kilimo cha Pamba hapa nchini badala ya kupoteza fedha zake nyingi katika kendesha vikao vinavyohusu zao hilo.

Ombi hilo lilitolewa juzi na Meneja wa Kiwanda cha Kahama oil Mil Wiliam Matonange wakati akizungumza na waandishi wa habari juu Kilimo cha mkataba ambacho wao kama wanunuzi wa zao hilo hawakubaliani nacho.

Matonange alisema kuwa Wakulima kwa sasa wanakuwa na wakati Mgumu wa kulima zao hilo kutokana na kuwa hawana dhamana na kuweka katika makampuni ya ununuzi wa zao hilo ili waweze kukopesheka.

Aidha Meneja huyo aliendelea kusema wao kama makampuni ya ununuzi wa zao hilo wanashindwa kuwakopesha wakulima hao na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo ni lazima kufunga nao mkataba.

“Ukifanya kilimo cha Mkataba na Wakulima ni sawa na kujitia hasara kwani Wakulima wanachotegea ni hali ya hewa ya wakati huo hali ambayo kama mvua ikikataa kunyesha itakuwa hasara kwa Kampuni”, Alisema Matonge

Akizungumzia kuhusu kukamatwa na kuwekwa ndani kwa kutuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Magalula kuwa makampuni hayo yamekuwa yakiwaibia wakulima Meneja alisema kuwa madai yake sii ya kweli.

Ilidaiwa mkutano wa Wanunuzi wa zao la Pamba uliofanyika Mkoani Geita kuwa baadhi ya Makampuni yaliokopeshwa mbegu na viwadudu na Bodi ya Pamba kwa nia ya kuwakopesha wakulima hawakufanya hivyo badala yake waliwauzia wakulima  hao kwa asilimia mia.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Magalula alisema kuwa kuna baadhi ya Makampuni yaliopewa mbegu hizo na Viwadudu hayakuwakapopesha  wakulima kama walivyokubaliana katika kikao husika.

Magalula aliendelea kusema kuwa kuna baadhi ya Mawakala  ambao pia ni wanunuzi wa zao la Pamba walifanya kinyume na makubaliano ikiwemo Kampuni ya Kahama oil mil.


Mkuu wa mkoa wa Geita Saidi Magalula Akiongea na waandishi wa habari juu ya masuala ya maendeleo ya kipindi cha miaka miwili katika mkoa wake na juu ya suala zao la pamba na wanunuzi 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply