sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » SERIKALI YATENGA BILION 40.1 KWA AJILI YA KUSAMBAZA MAJI KATIKA VIJIJI SHINYANGA



Na  Mohab Dominick
Shinyanga.
March 20, 2014

SERIKALI YATENGA BILION 40.1 KWA AJILI YA KUSAMBAZA MAJI KATIKA VIJIJI SHINYANGA

SERIKAli  imetenga shilingi Billion 40.18 zitakazotumika  kusambaza huduma ya maji katika Vijiji 100 kutoka  mradi wa maji ya ziwa Victoria kwenda  wilaya nne za mikoa ya Shinyanga na Mwanza, Imeelezwa.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA) Mhandisi Sylvester Mahole wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya maji Mkoani hapa, jana

Mhandisi Mahole alisema Miradi hiyo ambayo ni ya awamu ya pili inatarajiwa kuanza kujengwa julai mwaka huu na inakadiliwa kukamilika juni 2019 na ujenzi wake unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya sekta ya maji nchini.

Mahole alisema jumla ya vijiji 150 kutoka wilaya za Kahama Shinyanga na Msalala Mkoani Shinyanga pamoja na wilaya za Kwimba na Misungwi Mkoani Mwanza vimeainishwa kupatiwa huduma ya maji ya bomba kutoka mradi wa maji ya ziwa Victoria.

Alisema awali  mpango huo  una lengo la kusambaza huduma ya maji katika vijiji 100 ambapo  utekelezaji wake  utaanza na vijiji 20 kwa kila halmashauri  na shughuli za  upanuzi wa mtandao wa usambazaji maji kutoka mradi wa maji ya ziwa Victoria kwenda katika vijiji 100 utajengwa kwa kipindi cha miaka mitano.

Akihutubia mkutano wa hadhara katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji  uliofanyika katika  kijiji cha Bubinza wilaya ya Kishapu Mkoani hapa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Ally  Rufunga  alisema asilimia 51 ya wakazi wa Mkoa wa Shinyanga  vijijini hupata huduma ya majisafi  na asilimia 58.5 kwa wakazi wa mijini hupata huduma hiyo.

Rufunga alisema katika mipango ya muda mrefu miji ya Isaka na Kagongwa inategemewa kunufaika na mpango wa kutoa maji ya ziwa Victoria kupeleka katika miji ya Tabora, Nzega na Igunga ambapo hivi sasa usanifu unaendelea.

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply