sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » CHAMA CHA WALIMU WILAYANI KAHAMA CHATOA WITO KWA WALIMU WAKE

  

Watumishi wa utawala katika chama cha walimu Tanzania Kanda ya magharibi wametakiwa kuwa faraja kwa walimu wanapofika ofisini kusikilizwa matatizo yao, hali ambayo itawafanya kujisikia vizuri katika huduma zitolewazo na chama hicho

Changamoto hiyo imetolewa mjini Kahama na mwenyekiti wa Chama cha walimu Tanzania tawi la Kahama Victor Tandise wakati akifunga kikao cha siku mbili cha watumishi hao kanda ya magharibi yenye mikoa minne ya Kigoma , shinyanga Simiyu na Tabora kilicho fanyika mjini Kahama.

Katika kikao hicho kilicho washillikisha makatibu wa mikoa na wilaya pamoja na makatibu muktasi wao, Tandise amesema ili walimu kuwaweka kwenye faraja ni lazima wapate huduma nzuri ya mapokezi katika ofisi za chama ambazo ziko nchi nzima.

Aidha Tandise amesema kuna baadhi ya waajiri kama wakurugenzi katika halmashauri ni wakorofi ambao huwakorofisha waalimu wakati wa kudai maslahi yao, hivyo huwa changanya kiasi ambacho ofisi za vyama ndio iwe faraja kwao.

Kabla ya hapo mwenyekiti wa kikao hicho ambae pia ni katibu CWT mkoa wa Shinyanga Bi Rehema Sitta, amesema watumishi hao katika siku mbili walizokaa wamejifunza mbinu mbalimbali ya kutoa huduma kwa walimu ingawa pia wamepitia mkataba wa hali bora ya kazi zao za kila siku  na kufanyia marekebisho.

Kikao hicho pia kimeipitisha wilaya ya Kahama kuwa ndio kituo cha kufanyia vikao vyao kwa watumishi hao kutoka kanda hiyo ya magharibi, yenye mikoa hiyo mine.

Na Mohab Dominick-kahama

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply