sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » WARUNDI 19 WAKAMATWA BUKOMBE MKOANI GEITA


 Mkuu wa wilaya ya bukombe Amani mwenegoha akitoa ufafanuzi juu ya suala wahamiaji haramu katika wilaya yake amesema kuwa kuna baadhi ya watanzania wanatafuta vijana toka nchi jirani za rwanda na burundi kwenda tabora kwenye mashaba ya tumbaku .
 Baadhi ya wahamiaji haramu wakiwa chini ya ulinzi

 Baadhi ya wahamiaji haramu wakiwa ofisi za uhamiaji wilayani bukombe
 Mkuu wa wilaya ya bukombe hakitoa ufafanuzi juu ya ulinzi shirikishi kwa jamii ofisini kwake wakati akiongea na wanahabari ofisini kwake .


Na Mohab Dominick
Sept 14,2014
GEITA-BUKOMBE,

WARUNDI 19 wamekamatwa mjini Ushirombo Wilayani Bukombe mkoani Geita wakiwa kwenye gari aina ya Hiace wakielekea  Mkoani Tabora,
 mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkuu wa wilaya ya Bukombe Amani mwenegoha amewaeleza waandishi wa habari kuwa jeshi la polisi likiwa kwenye msako maalumu kufuatia tukio la majambazi kuvamia kituo cha polisi kisha kuua askali wawili na kupora siraha zaidi ya kumi yakiwemo mabomu ya machozi.

Amesema mpaka sasa wameshawakamata watanzania wawili ambao wanafanya biashara ya kuwaingiza warundi kinyemela kwa kile walichodai kuwa wanaenda mkoani Tabora kwa ajili ya kuwatumikisha kama vibarua kwenye mashamba ya Tumbaku.

Mwenegoha amesema kuwa tabia hiyo ya kuwaingiza warundi  ni hatari kwa Taifa kwani watu hao huwa si wema kwani  wanapoingia na kutumikishwa kama manamba hawaoni shida lakini madhara yake huja baadae pindi wakizoea na kusoma mazingira kwani wakimaliza shughuli za kilimo na mavuno hurudi kwao  na kuwaleta wenzao kisha kuanza kazi ya uvamizi. 

Mkuu huyo amesema warundi hao kesho watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka  ya kosa la kuingia nchini bila kibari na watanzania hao wawili kwa kosa  la kuwaingiza watu kuja kuishi nchini bila ya kibari halali,

Aidha mkuu huyo wa wilaya ametoa wito kwa wananchi waache tabia ya kwenda nchi jirani kusaka vibarua na kuwaingiza nchini pia ametoa donge nono la shilingi laki moja kwa yeyote atayetoa taarifa sahihi kumpata jangili, jambazi mwenye siraha na wahamiaji haramu. 

 Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply