sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » KAMATI YA LEMBELI YAMPA MIEZI MITATU WAZIRI MWENYE DHAMANA YA MAZINGIRA KUIBANA MIGODI

 Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika ziara ya kutembelea migodi ya dhahabu na kamati ya mazingira ,ardhi nyumba na maendeleo katika mgodi wa buzwagi .
 Mmoja wa watalamu  wa kigeni akiwakaribisha baadhi ya wana habari katika ziara ya kamati ya mazingira .

 kamati ya Bunge Ardhi maliasili na mazingira wakiwasili katika mgodi wa buzwagi wilayani kahama .
 Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi maliasili na mazingira mh  James Lembeli.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya bunge ya ardhi maliasi na mazingira wakipewa maelezo toka kwa meneja wa mgodi wa buzwagi Filbert Rweyemamu Wakati kamati hiyo ilipotembelea mgodi huu .

 Naibu waziri  Ofisi ya makamu wa Rais mazingira  (omr )ummy mwalimu mwenye miwani kifuani wakiwa katika ukumbi wa mgodi wa dhahabu wa buzwagi wakati kamati hiyo ilipotembelea mgodi huu .
 Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakibadilisha mawanzo kabla ya kamati ya mazingira kuwasili katika mgodi huu.

 Mmoja ya Dappa la kubeba mawe ya dhahabu  nakupelekwa kwenye kinu cha kuvunja mawe ambapo gari hilo  linauwenzo wa kubeba tani 150  za mawe hayo ya dhahabu .
 Wajumbe wa kamati ya Ardhi  maliasili na mazingira wakiangalia moja ya bwawa la kupokea maji toka ziwa victori ambapo bwawa hilo limejingwa kwa kiwango kikubwa .
 Mmoja ya jengo la kituo  cha Afya mwendakulima ambapo mgodi wa buzwagi hunafadhili kwa gharama nafuu.
 Wajumbe wa kamati ya bunge Ardhi maliasili na mazingira wakitoka katika moja ya bwawa la sumu ya cyanide .
 Hili ndiyo bwawa lenye sumu ya Cyanide ambalo limeifaziwa kwa umaki mkubwa katika eneo hilo .
 Moja ya gari la kumwanga maji kwa ajili ya kuondoa vumbi la mchanga wa mawe ya dhahabu .
 Mwenyekiti wa kamati ya  Ardhi maliasili na mazingira Mh James Lembeli Akiongea na meneja wa mgodi wa buzwagi Filbert Rweyemamu na muandishi wa habari za mazingira Jacob Rusungu katika mgodi wa buzwagi .
 Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi mazingira  Mh James Lembeli akiwa kwenye picha ya pamoja na muandishi wa habari za uchumi Herman Meza Mwenye miwani mnyeusi  pamoja na wajumbe wa kamati hiyo .
 Mwenyekiti wa kamati ya Ardhi maliasili na mazingira Mh James Lembeli Mwenye miwani Akipewa maelezo toka kwa meneja mkuu wa  mgodi wa Buzwagi Firbert Rweyemamu mwenye karatas nyeupe .
 
 Baadhi wa wajumbe wa kamati ya Ardhi maliasili na mazingira wakiwasili katika mgodi wa buzwagi .
 Mmoja ya mtambo mkubwa wa kupokea maji toka ziwa victoria ambao hunaingiza maji  hayo katika mgodi huu
 Meneja mkuu wa Mgodi wa Dhahabu Buzwagi Filbert Rweyemamu akizumgumza na wajumbe wa kamati ya bunge ya mazingira .
Wajumbe wa kamati ya bunge ya mazingira wakitoka maeneo  kukangua  sehemu mbalimbali  za utunzaji wa mazingira katika mgodi huo.

Kamati ya Bunge ya ardhi,maliasili na mazingira imempa miezi mitatu waziri wa nchi ofisi ya  Makamu wa Rais mazingira kufuatilia uzingatiaji wa sheria na kanuni za kuhifadhi mazingira katika migodi yote nchini.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. James Lembeli alitoa maagizo hayo kwa Waziri mwenye dhamana hiyo Mhe.Ummy Mwalimu  mgodini  Buzwagi   baada ya kuhitimisha  ziara ya kukagua migodi hiyo kanda ya ziwa jana.

Mhe.Lembeli alisema kuwa hali ya usalama,hifadhi ya mazingira na utekelezaji wa sheria na kanuni husika si nzuri kwa baadhi ya migodi nchini jambo linalohatarisha usalama wa Binadamu na viumbe hai.

Hata hivyo alitoa sifa za kipekee kwa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi kwa namna ulivyopokea na kufanyia kazi maagizo yote ya Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC) hususani kulinda na kuhifadhi taka sumu zitokazo mgodini zisiingie katika vyanzo vya maji.

Mhe.Lembeli alisema kuwa kamati yake imeridhika kuona kila kitu kimewekwa kwa mpangilio bora kwa tahadhari na hali ya usalama ikiwamo ulipuaji miamba na uhifadhi wa kemikali hatari zitumikazo kuchanjua dhahabu. 

Akijibu hoja hiyo waziri mwenye dhamana hiyo katika ofisi ya makamu wa Rais , Ummy Mwalimu aliahidi kutumia taasisi zote husika chini ya ofisi yake ikiwamo NEMC,kukagua utekelezaji wa maagizo ya kamati hiyo ya Bunge.

“Mhe.Mwenyekiti ndani ya miezi mitatu tutafuatilia na kutoa taarifa katika kamati hii kuhusu utekelezaji wa maagizo ya NEMC kwa migodi yote nchini kuhakikisha inazingatia sheria na kanuni husika.”Alisema waziri Mwalimu.

Akijibu hoja za Kamati ya Bunge mkurugenzi mkuu wa NEMC Eng.Bunaventure Baya alisema ameridhika namna mgodi wa Buzwagi ulivyotekeleza maagizo ya Baraza hilo na hatimaye kupewa hati maalum ya kutambua jitihada hizo.

Naye meneja mkuu wa mgodi huo Filbert Rweyemamu alisema kuwa mgodi huo ulipokea malalamiko 36 toka kwa jamii inayozunguka mgodi huo na kutatua 33 ambapo tatu zilizo baki zinaendelea kutafutiwa ufumbuzi. 

MWISHO

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply