sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» » » MWENYEKITI MZALENDO FOUNDATION ATOA SALAAM ZA MWAKA



mwenyekiti wa Taasisi ya Mzalendo Foundation, Khamisi Mgeja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake mjini Kahama wakati akitoa salaam zake za kheri ya mwaka mpya wa 2015.


Ushauri huo umetolewa jana na mwenyekiti wa Taasisi ya Mzalendo Foundation, Khamisi Mgeja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake mjini Kahama wakati akitoa salaam zake za kheri ya mwaka mpya wa 2015.

Mgeja alisema wakati taifa likiingia katika kipindi kingine cha mwaka 2015 kuna umuhimu mkubwa wa mihimili mikubwa mitatu hapa nchini ikatanguliza mbele suala la utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia mipaka yake kama ilivyoainishwa ndani ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuepuka migongano isiyo ya lazima.

Alisema zipo dalili zilizoanza kujitokeza kwa mihimili hiyo mikuu kuanza kuingiliana na kupingana katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku hali ambayo inaweza kuchangia kuharibu mstakabali wa kiutawala na hivyo nchi kujikuta ikiingia katika mtikisiko mkubwa.

Mwenyekiti huyo alisema katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 toleo la 2005 imeainisha wazi utekelezaji wa shughuli za mamlaka ya nchi katika ibara yake ya nne vifungu vidogo vya (1) na (2) hivyo ni muhimu kwa kila mhimili ikaheshimu katiba hiyo ya nchi.

“Kifungu kidogo cha (2) kinaeleza kuwa, vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, vyombo  vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki vitakuwa ni Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na;”

“Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni Bunge na Baraza la Wawakilishi, utaona wazi kila mhimili umeainishiwa majukumu yake,” alieleza Mgeja.

Mgeja alitahadharisha migongano ya kimihimili nchini kwamba isipochukuliwa tahadhari ya kila mhimili kuheshimu eneo la mhimili mwingine kama ilivyowahi kutokea kipindi cha Spika wa bunge lililopita la 2005/2010, Samwel Sitta na hivi karibuni katika bunge la juzi lilipokuwa likijadili suala la akaunti ya Tegeta Escrow.

“Wakati wa kipindi cha Spika Sitta (Samwel) tuliona ilivyotaka kutokea kwa mihimili kutaka kuingiliana na kusababisha mtafaruku mkubwa, lakini nihivi karibuni katika bunge lilopita   tulimsikia mama yenu Anne Makinda akilalamika na kuwa wasihi  wabunge wasimsababishie atakuwa mgeni wanani katika mihimili  mingine   ,”

“Binafsi napenda kushauri wakati tukiuanza mwaka huu wa 2015 na kuuaga mwaka 2014 ni vyema watanzania tukahakikisha nchi yetu inaendelea kuwa na amani na utulivu tulionao, na tuwaombe viongozi wetu wa madhehebu mbalimbali ya kidini waongeze maombi yao katika kuiombea amani nchi yetu,” alieleza Mgeja.

Kwa upande mwingine Mgeja ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga ameishauri serikali iangalie uwezekano wa kuanzisha vyuo maalumu vitakavyotoa mafunzo ya kiuongozi ili kuiwezesha nchi iwe ikipata viongozi waliopitia mafunzo hayo.

Alisema kuanzishwa kwa vyuo hivyo ni muhimu katika kipindi hiki na jambo la lazima kwa vile vitasaidia kupatikana kwa viongozi waadilifu wenye kuheshimu miiko ya kiuongozi na kuelewa nini wajibu wao kwa umma uliowachagua kuwaongoza.

“Ukweli mara nyingi tumekuwa tukiwalaumu bure viongozi wetu tunaowakabidhi jukumu la kuongoza nafasi mbalimbali za kiutawala , wengi wao tunawabebesha majukumu makubwa kuliko uwezo walionao, uongozi siyo jambo la kufanyia majaribio, nchi kuwa na viongozi ambao hawajaandaliwa juu ya utekelezaji wa majukumu yao kama viongozi, ni majanga, ni muhimu wakaandaliwa,” alieleza Mgeja.

Mwisho.





«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply