sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » CHADEMA KAHAMA WAKAMATISHANA RUSHWA.




Kahama
18, 2013.



UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)Wilaya ya Kahama juzi umekemea vikali tabia iliyofanywa na Mwenyekiti wa baraza la uongozi wa Wilaya la kula Rushwa ili kuwatoa wanachama wa chama hicho waliokuwa wamekamatwa na kuwekwa mahabusu kwa tuhuma za kuwazuia watumishi wa Serikali kufanya kazi.

Akiongea mbele ya Waandishi wa habari mjini Kahama Mwenyekiti wa baraza la vijana la Chadema ( BAVICHA) Benedict Shija  alisema kuwa kitendo kilichofanywa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Juma Protasi la kupokea Rushwa ya shilingi 75,000 kutoka kwa ndugu wa watuhumiwa ni cha kulaaniwa vikali na kinyume cha katiba ya chama hicho.

Alisema kuwa sakata la kukamatwa na Rushwa kwa kiongozi huyo lilikuja baada ya kukamatwa watuhumiwa Elias Mayunga ambaye ni Mwenyekiti wa Chama hicho kata ya Kilago pamoja na Katibu wake Daniel Makoye ambao walikuwa wakishikiliwa na Jeshi la polisi kwa makosa ya kuwazuia maafisa wa Serikali kufanya kazi zao katika kata hiyo.

Alisema kuwa kufuatia Watuhumiwa kukamatwa na kukaa mahabusu kwa muda wa siku 14 ndipo Mwenyekiti huyo alipowafuta ndugu wa watuhumiwa hao na kuomba kiasi hicho cha fedha ili aweze kuwatoa Mahabusu watumiwa hao huku yeye akihaidi kuongeza kiasi cha shilingi 40,000 kama kuwaunga mkono wanachama wake katika kufanikisha dhamana yao Mahakamani.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo baada ya kupokea kiasi hicho cha fedha Juma Protasi aliamua kuzila fedha hizo huku akidai kuwa watuhumiwa hao wangetoka  siku inayofuata hali ambayo haikuweza kutekelezeka na ndipo baadhi ya wanachama wa Chadema Jimbo la Kahama walipoamua kuingilia kati suala hilo hilo huku wakimtaka kurudisha fedha hizo kwa wahusika kwani dhamana ya watuhumiwa hao ilikuwa haihitaji fedha  yeyote.

Shija alisema kuwa baada ya wanachama kuchachamaa ndipo Mwenyekiti huyo alipoamua kufuata fedha hizo nyumbani kwake na kufanikiwa kurudisha kiasi cha shilingi 70,000 kati ya 75,000 alizochukua hali ambayo ilifanya wanachama hao kufikisha suala hilo katika taasisi ya kuzua na kupambana na Rushwa (PCCB).

Kwa upande wake Mwenyekiti huyo Juma Protasi alipotafutwa na Waandishi wa habari kwa ajili ya kuthibisha tukio hilo hakuweza kupatikana na hata alipopigiwa simu ya kiganjani simu yake ilikuwa ikiiita bila ya kuwa na majibu yeyote.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Kahama Barikiel Israel alisema kuwa kwa sasa wanajiandaa kuitisha Kikao cha Kamati tendaji ya jimbo kwa ajili kujadili suala hilo kabla ya kulifikisha katika uongozi wa Mkoa kwa hatua za kinidhamu zaidi.

Pia alitoa wito kwa Viongozi wa Chama hicho wasiwe na tamaa bali wafanye kazi kwa kufuata katiba ya Chadema kwani chama hicho kina sera ya kupinga Rushwa na sii kuona viongozi wake wanakuwa katika mastari wa mbele katika kula Rushwa tena kwa wanachama wake wenyewe.

Mwisho.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply