sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » SABABU YA MBEGU ZA QUTONI KUTOOTA ZABAINISHWA



Na  
Kahama
Des 22, 2013.
 

IIMEELEZWA kuwa sababu kubwa ya Mbegu za Pamba za Quton kutoota ni kutokana na kampuni hiyo kuchuka mbegu kwa Wakulima ambazo tayari zinakuwa zimetiliwa maji kwa kiasi kikubwa badala ya kutumia zile ambazo zimetoka katika mashamba ya mbegu.

Hayo yalibainika juzi wakati wa Madahalo kuhusu kilimo cha Pamba ulioandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la kutetea na kuimarisha Demokrasia pamoja na utawala Bora (ADLG) ambapo baadhi ya wakulima wa zap la Pamba walipata fursa ya kuchangia.

Akiongea kwa niaba ya Makapuni ya ununuzi wa zao la Pamba Wilayani Kahama Edson Peter Mwakilishi kutoka kampuni ya NIDA textile alisema kuwa kampuni ya quton imekuwa ikinunua mbegu za pamba kutoka wakulima badala ya kutoa katika mashamba darasa ya mfano wanayotakiwa kulimwa.

Peter alisema kuwa kwa mujibu wa Sheria msambazaji wa mbegu za Pamba anatakiwa kuwa na Shamba darasa kwa ajili ya Mbegu za Pamba hali ambayo kampuni hiyo imekuwa kinunua mbegu kutoka kwa wakulima ambazo tayari zinakuwa hazina ubora.

“Ukitaka kuamini kuwa mbegu hizo hazina ubora hebu chukua mkasi na kasha zikate utaona hali ya majimaji ambayo tayari inashirikua mbegu hizo zimeoza hali ambayo kwa sasa imeleta mazozo mkubwa kwa wakulima wa Pamba kwani hazioti”, Alisema Edson Peter mwakilishi kutoka kampuni ya NIDA Texitile.

Pamoja mambo mengine yaliojadiliwa katika mdahalo huo ambao pia uliwajumuisha wakulima wa zao la Pamba maafisa kilimo kutoka Halmashauri tatu za Ushetu, Msalala pamoja na mji pia walijadili juu ya serikali kuona umuhimu wa kuifuta bodi ya pamba kwa haina msaada kwa mkulima.

“Hivi bodi ya pamba haina muda wake na kwa nini serikali isiifute bodi hiyo kwani haitusaidii kwa chochote ni bora ikawa hata muda wa kuongoza ili watu wawe wanabadilishana kwa nia ya kumuinua kulima wa Pamba”, Alisema Peter.

Mmoja wa wakulima wa Pamba kutoka katika Wilayani hapa Maimuna Saidi alisema kutokana na upungufu mkubwa wa maafisa ugani uliopo ni bora serikali ikatumia vijana waliomaliza kidato cha nne mwaka uliopita ukawapa mafunzo ya muda mufupia kwa nia ya kuwaelimisha wakulima wa Pamba juu ya zao hilo.

Alisema kuwa kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa maafisa ugani katika maeneo wanayolima Pamba hali ambayo inafanya wakulima wengine kufikiria kujitoa katika kulima zao la Pamba kwa kuwa wanaona kuwa zao hilo halina tija kwani wanatumia nguvu kubwa kulima huku mafanikio yakiwa ni madogo

mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply