sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Kimataifa Habari

habari

Habari Za Mastaa

Michezo

simulizi za kusisimua

» »Unlabelled » WACHIMBAJI WAIOMBA SERIKALI KUWAPA MAENEO YA KUCHIMBA DHAHABU TABORA



 MZEE MASUNGA AKIWAELEZA WANAHABARI NJISI ENEO LAKE LILOFUKIWA KWA AMRI YA MKUU WA WILAYA NA MOJA WA WACHIMBAJI MMOJA KUFARIKI DUNIA
 MTO MKUBWA HUNAOTENGANISHA ENEO LA MGODI WA DHAHABU WA RESOLUTE
 WACHIMBAJI WADOGOWADOGO WAKISILIZA MKUTANO WA HADHARA
 BAADHI YA WACHIMBAJI WAKISIKILZA MKUU WA WILAYA YA NZEGA KATIKA MKUTANO WA HADHARA
 AFISA UPELELEZI WA WILAYA YA NZEGA AKIONYESHA MKUU WA WILAYA YA NZEGA SEHEMU AMBAYO ILIFUKIWA CHINI YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA
MWENYEKITI WA KIJIJI CHA NHOBOLA AKITOA MALALAMIKO YAKE KWA MKUU WA WILAYA YA NZEGA KATIKA MKUTANO WA HADHARA  BITINI MSANGI KUHUSU KUFUKUNZWA KATIKA MAENEO YAO
mkuu wa wilaya ya nzega Bitini msangi Akiongea na wachimbaji wadogo dogo  katika kijiji cha Nhobola wilayani nzega 


Nzega
Jan  3, 2014.
 

WACHIMBAJI wa dogo wa Dhahabu katika machimbo madogo ya mwanshina katika kijiji cha Nhobola wilayani Nzega Mkoani Tabora,wameiomba serikali kuwapatia ridhaa ya kuchimba dhahabu pembezoni mwa mgodi mkubwa wa dhahabu wa Resolute ili wakidhi mahitaji yao ya msingi.

Wakizungumza katika mkutano wa kijiji mbele ya mkuu wa wilaya ya Nzega Bituni  Msangi walisema kuwa serikali kupitia waziri wa NishatI na madini wamewaomba kuwapatia ridhaa ya kuendelea na shuguli hizo za uchimbaji wa dhahabu pembezoni mwa mgodi wa resolute kwa kuwa mwekezaji huyo muda wake unaishia mwaka 2015.

Mwenyekiti wa wachimbaji hao Joseph Mabondo alisema kuwa mgogoro uliopo kati ya serikali na wachimbaji ni kutokana na wachimbaji kukosa eneo la kuchimba dhahabu huku wawekezaji hao wakiwa na eneo kubwa ambalo halitumiki hali inayo sababisha wachimbaji hao wadogo kukosa sehem ya kuchimba iliwajipatie ridhiki.

Joseph aliiomba serikali isikie kilio hicho kikubwa cha wachimbaji hao ambapo ni wakazi wa pembezoni na mgodi huo iliwaweze kupatiwa kibali cha kuchimba dhahabu kwa uhuru kama baadhi ya sehem nyingine jinsi wa chimbaji wadogo wanavyo endelea na shuguli zao.

Alisema kuwa kitendo cha kuwa piga marufuku na kuwafukuza katika machimbo hayo nikusababisha mahusiano mabaya kati ya wachimbaji na serikali na kuongeza kuwa wachimbaji hao wana haki ya kupewa nafasi ya kuchimba ili kukidhi mahitaji yao ikiwa na kukuza uchumi wa ndani ya wilaya hiyo.

‘’sisi siyo wakimbizi ndani ya nchi hii ni wazawa kabisa tuna muomba waziri husika na naibu wake masele watusaidie suala hili ili tuweze kujikidhi mahitaji yetu mambo ya kukimbizana na kufukuzana sio vizuri serikali tutizameni kwa macho mawili na sisi tunufaike na rasilimali zetu’’,alisema Joseph mabondo.

Alisema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya wawekezaji wamekuwa wakimiliki maeneo makubwa huku wakiwa hawayatumii katika shughuli zao za uchimbaji hali ambayo kwa wachimbaji wadogo wakipewa maeneo hayo wanaweza kuyaendeza kwa haraka zaidi.

‘Mwekezaji huyo wa mgodi wa Resolute muda wake unaisha mwakani 2015 na kwa sasa hakuna shughuli zozote za uzalishaji zinazoendelea katika mgodi huo mkwani hili eno lililobaki tusipewe sisi wachimbaji wadogo tulio katika jirani na mgodi huu “Alisema Mwenyekiti huyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nzega Bitini Msangi alisema kuwa kuwa kilio cha Wachimbaji wadogo katika eneo hilo amekisikia na kuhaidi kuwa suala  hilo atalifanyia kazi yeye kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya nzega huku lengo kubwa likiwa ni kumshawishi mwekezaji wa Mgodi huo kuwapa eneo hilo wachimbaji wadogo ili kuweza kulifanyia kazi katika shughuli za uchimbaji.

mwisho


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply